Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Lucy Oduor (kushoto) na Irene Wambui (kulia) wakiwa katika eneo lao la biashara huko Ngong lililo katika kaunti ya Kajiado nchini Kenya.
UN News

Biashara ndogo ndogo yakwamua wanawake na vijana kiuchumi Kajiado nchini Kenya

Wiki hii Ijumaa tarehe 8 Machi 2024, ulimwengu utaadhimisha Siku ya Wanawake Duniani ambapo mwaka huu ina maudhui “Wekeza kwa wanawake: Harakisha maendeleo,” lakini Shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya wanawake, UN Women linasema ni dhahiri kwamba ulimwengu bado unakabiliwa na migogoro mingi, kuanzia mizozo ya kijiografia hadi viwango vya umaskini vinavyoongezeka, ukosefu wa usawa na kuongezeka kwa athari za mabadiliko ya tabianchi. 

Audio Duration
4'19"
Huduma za kibinadamu na haki za binadamu zazidi kutwama nchini Haiti..
© UNICEF/Ndiaga Seck

Haiti: Huduma za kibinadamu na haki za binadamu zazidi kutwama

Kutoroka gerezani kwa zaidi ya wafungwa 4,500 nchini Haiti mwishoni mwa wiki iliyopita wakiwemo viongozi mashuhuri wa magenge ya uhalifu kukitajwa kuwa tishio la usalama wa taifa, huku huduma muhimu kama afya, elimu zikiendelea kuzorota kila uchao, Umoja wa Mataifa unataka hatua za haraka za jamii ya kimataifa kuzuia taifa hilo kuzidi kutumbukia kwenye ghasia.

Dawa za kulevya za aina ya Cocaine zanaswa katika Bandari ya Kingston, Jamaika, mnamo Machi 2023.
© UNODC

Ongezeko la mihadarati mtandaoni INCB yaja na suluhu

Walanguzi wa mihadarati wanaendelea kutumia teknolojia za kidijitali, mitandao ya kijamii na taarifa potofu kuuza biashara zao haramu na kuchochea matumizi ya mihadarati au dawa za kulevya duniani imesema ripoti mpya iliyozinduliwa leo ambayo inaungwa mkono na Umoja wa Mataifa.

Margerita, Mwanamke mkulima nchini Sudan Kusini, anapanda mbegu za zao la mahindi. (Maktaba)
FAO/Jean Di Marino

Joto na mafuriko huathiri wanawake na wanaume wa vijijini tofauti na kuongeza tofauti ya kipato

Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO limezitaka nchi kuhakikisha zinashughulikia changamoto za usawa wa kijinsia kwenye kupambana na madhara ya mabadiliko ya tabianchi kwani takwimu zinaonesha kuwa familia hususan za vijijini zinazoongozwa na wanawake zinaathirika zaidi na mabadiliko ya tabianchi ikilinganishwa na zile zinazoongozwa na wanaume.