Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Uvutaji wa tumbaku unaunaathiri afya yako.
© Unsplash/Andres Siimon

Nilivuta sigara tangu mtoto, acheni haina maana- Thierry

Nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, simulizi ya mtu aliyeanza kuvuta sigara akiwa kijana balehe na sasa ameamua kuacha inamulika ni kwa nini shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani, WHO linasisitiza umuhimu wa kampeni za kuacha tumbaku kwani ni miongoni mwa visababishi vikubwa vya maambukizi ya saratani ya mapafu inayooongoza kwa kuua zaidi vifo miongoni mwa wanaume duniani. 

Sauti
2'26"
Maria Ondosia Mawero, mama mzee kutoka Kenya ambaye ameishi maisha ya upweke kwa muda mrefu. Sasa anasikiliza mahubiri na muziki wa kanisa kupitia redio na mara nyingi hukutana na marafiki ili kupunguza upweke.
WHO

Uhusiano wa kijamii huondoa upweke na kuboresha afya kwa jamii – WHO

Mwezi Novemba mwaka jana shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO lilizindua Kamisheni  ya kuchochea Muunganisho wa Kijamii au Social Connection kwa lengo la kuondokana na tatizo la upweke ambalo limetambuliwa kuwa moja ya tishio kubwa la afya duniani. WHO inasema kutengwa na jamii na kuishi maisha ya upweke ni jambo hatari, chungu, na zaidi hatari kwa afya ya binadamu.

Sauti
4'6"
Maonesho ya bidhaa za kupambana na saratani kwenye kongamano la kwanza la taifa la saratani nchini Kenya.
UN News Nairobi/Thelma Mwadzaya

Licha ya kuweko kwa mbinu za kudhibiti, bado saratani yaendelea kuwa mzigo wa afya duniani

Takwimu mpya za Umoja wa Mataifa zinaonesha kuwa ugonjwa wa saratani umeendelea kuwa mzigo kubwa wa afya duniani na kusababisha vifo licha ya kuweko kwa mbinu za ugunduzi na matibabu, huku saratani  ya mapafu ikishika nafasi ya kwanza na ile ya titi ikishika nafasi ya pili na wadau wakitaka utashi wa kisiasa ili kutokomeza ugonjwa huo.

Timu za UNRWA zinaendelea kusambaza misaada ya kibinadamu huko Gaza.
© UNRWA

Habari kwa ufupi: Msaada wa kibinadamu Gaza; Wandishi wa Habari; Saratani

Kufuatia uamuzi wa nchi 16 wafadhili kusitisha utoaji fedha kwa shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia wakimbizi wa kipalestina UNRWA baada ya Israel kulishutumu shirika hilo kuwa wafanyakazi wake 12 walihusika katika shambulio lililotokea tarehe 7 Oktoba mwaka jana, Mkuu wa UNRWA Philipe Lazzarini amesema kuwa iwapo fedha zitaendelea kuzuiliwa, watalazimika kufunga operesheni zao ifikapo mwishoni mwa mwezi huu wa Februari.