Rafah ikilengwa itakuwa ni mauaji - OCHA
Operesheni za jeshi la Israel huko Rafah, “zinaweza kusababisha mauaji na kudumaza kazi ya kuokoa maisha zinazofanyika Gaza, imesema hii lwo ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya dharura, OCHA.
Operesheni za jeshi la Israel huko Rafah, “zinaweza kusababisha mauaji na kudumaza kazi ya kuokoa maisha zinazofanyika Gaza, imesema hii lwo ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya dharura, OCHA.
Leo ni siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani mwaka huu ikibeba maudhui “Vyombo vya Habari kwa ajili ya Sayari: Uandishi wa habari katika kukabiliana na mgogoro wa mabadiliko ya tabianchi” kwani Umoja wa Mataifa unasema mchango wa wanahabari na vyombo vya habari ni kiini katika kuhabarisha na kuelimisha umma kuhusu changamoto hiyo ya tabianchi.
Tukiwa katika msimu wa mvua kwa nchi nyingi za kusini mwa jangwa la Sahara, tuelekee nchini Somalia, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura, OCHA limesema wao na wadau wao wamejiandaa kufikisha mahitaji kwa watu 770,000 katika wilaya 22 za nchi hiyo ambao wanatarajiwa kuathirika na mvua za msimu huku wakieleza kuwa wakimbizi wa ndani wanatarajiwa kuaahirika ziadi.
Hii leo ni siku ya kimataifa ya uhuru wa vyombo vya habari maudhui yakiwa Uandishi wa Habari wakati huu wa janga la mazingira ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO kwa kushirikiana na shirikisho la waandishi wa habari duniani, IFJ wametoa ripoti yao ikionesha kuwa ni katika kipindi cha miaka 15 iliyopita waandishi wa habari 44 waliuawa wakiwa wanachunguza masuala ya mazingira. Kampeni ya siku hii ni kwamba kila habari kuhusu mazingira lazima isimuliwe hivyo waandishi wa habari walindwe.
Niger ambayo mwaka huu inakabiliwa na ongezeko la asilimia 50 la wagonjwa wa uti wa mgongo au meningitis ikilinganishwa na mwaka jana, limesema shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO.
Kamati ya michuano ya Olympic imeitangaza rasmi hii leo timu ya wachezaji wakimbizi 36 kutoka nchi 11 ambao wanashiriki katika michuano ya mwaka huu huko Paris Ufaransa ambao wanatarajiwa kushirikia katika michezo 12.
Katika hatua inayotia wasiwasi Gaza , Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masuala ya kibinadamu na misaada ya dharira OCHA imesema zaidi ya watu 10,000 wanaaminika kuzikwa chini ya vifusi.
Hii leo tunakukutanisha na wanawake waandishi wa habari nchini Somalia wanaoendesha chombo chao kiitwacho Bilan. Chombo hiki kilianzishwa mwezi Aprili mwaka 2022 ili kuwapatia wanawake waandishi wa habari nguvu thabiti na ya ukweli pamoja na fursa ya kusongesha habari mpya na sauti mpya kwa hadhira nchini mwao Somalia.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema amesikitishwa sana kusikia mamia ya watu wameopoteza maisha na wengine wengi kuathiriwa na mafuriko makubwa katika nchi za Burundi, Kenya, Somalia na Tanzania na maeneo mengine ya Afrika Mashariki.
Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani WHO imesema kuna uhusiano baina ya COVID-19 na Watoto kukabiliwa na changamoto ya utipwatipwa au obesity barani Ulanya.