Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Baadhi yao wamepumzika baada ya siku yenye shughuli nyingi kwenye Mkutano wa Viongozi wa Dunia.
UN News/Laura Quinones

Wanahabari wana jukumu muhimu la kuelimisha juu ya mabadiliko ya tabianchi: UN

Leo ni siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani mwaka huu ikibeba maudhui “Vyombo vya Habari kwa ajili ya Sayari: Uandishi wa habari katika kukabiliana na mgogoro wa mabadiliko ya tabianchi”  kwani Umoja wa Mataifa unasema mchango wa wanahabari na vyombo vya habari ni kiini katika kuhabarisha na kuelimisha umma kuhusu changamoto hiyo ya tabianchi. 

Sauti
2'23"
Mwanamke akipita kwenye maji ya mafuriko katika Jimbo la Hirshabelle, Somalia.
© WFP/Arete/Abdirahman Yussuf Mohamud

OCHA na wadau waanza kufikisha misaada kwa wakimbizi ili kujiandaa na mafuriko

Tukiwa katika msimu wa mvua kwa nchi nyingi za kusini mwa jangwa la Sahara, tuelekee nchini Somalia, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura, OCHA limesema wao na wadau wao wamejiandaa kufikisha mahitaji kwa watu 770,000 katika wilaya 22 za nchi hiyo ambao wanatarajiwa kuathirika na mvua za msimu huku wakieleza kuwa wakimbizi wa ndani wanatarajiwa kuaahirika ziadi. 

Sauti
2'17"
Mtoto akiwa juu ya lundo la mchanga ambao hutumiwa na wakazi wa eneo hili kujaribu kuzuia maji ya ziwa Albert yasiingie kwenye makazi yao.
UN/ John Kibego

Waandishi wa habari 44 waliuawa wakichunguza masuala ya mazingira

Hii leo ni siku ya kimataifa ya uhuru wa vyombo vya habari maudhui yakiwa Uandishi wa Habari wakati huu wa janga la mazingira ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO kwa kushirikiana na shirikisho la waandishi wa habari duniani, IFJ wametoa ripoti yao ikionesha kuwa ni katika kipindi cha miaka 15 iliyopita waandishi wa habari 44 waliuawa wakiwa wanachunguza masuala ya mazingira. Kampeni ya siku hii ni kwamba kila habari kuhusu mazingira lazima isimuliwe hivyo waandishi wa habari walindwe.

Sauti
3'13"