Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Zahra K Salehe Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji, ICCAO Tanzania akizungumza na wanafunzi.
UN News

ICCAO Tanzania: Shirika la vijana linalosaidia kufanikisha SDGs nchini Tanzania

Mnamo tarehe Mosi Januari mwaka 2016, Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu (SDGs) yalianza kufanyiwa kazi rasmi. Tangu wakati huo watu ulimwenguni kote kwa ngazi tofautifauti wamekuwa wakihaha kuhakikisha kufikia mwaka 2030 malengo hayo yanafikiwa. Na kila mara Makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani yamekuwa uwanja wa wazi kwa wadau kutoka kila pembe ya dunia kuja katika mikutano mbalimbali na kubadilishana uzoefu. 

Sauti
5'17"
Watu wakichota maji ya kunywa huko Rafah kusini mwa Gaza
© UNRWA

Gaza: Huko Rafah hofu yatanda, wagonjwa wahofia kusaka huduma

Hofu kubwa ikiendelea kutanda huko Rafah, kusini mwa Gaza wakati huu ikiripotiwa kuwa Israel inataka kuelekeza operesheni zake za kijeshi kwenye eneo hilo, shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni ,WHO linasema hospitali tayari zimezidiwa uwezo kwani Umoja wa Mataifa umekuwa unasema operesheni hiyo ya kijeshi itasababisha idadi kubwa ya vifo na majeruhi ambao watahitaji huduma za afya.