Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres (Kushoto) na waziri wa mambo ya nje wa Misri Sameh Hassan Shoukry Selim mjini Cairo
UN Photo/Eskinder Debebe

Madai halali hayawezi kuhalalisha ugaidi, na ugaidi hauwezi kuhalalisha adhabu ya pamoja: Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ambaye yuko Cairo Misri  amekutana na Waziri wa Mambo ya Nje w anchi hiyo Sameh Shoukry na kisha kuzungumza kwa pamoja na na waandishi wa habari akisema yuko ziarani Mashariki ya Kati kuona misaada ya kibinadamu inayohitajika inawasilishwa kwa wahitaji huko Ukanda wa Gaza kupitia kivuko cha Rafah. 

Lori likiwa limejaa chupa za maji ya kunywa  likielekea Al Arish mji ulio kilometa 32 kusini mwa mpaka wa Gaza
© UNICEF/Mohamed Ragaa

Udadavuzi: Kuna nini ndani ya msafara wa misaada kwenye kivuko cha Gaza

Chini ya kilomita moja kutoka Gaza, vibao vya kuengeshean chakula, mafuta, maji, na dawa ni miongoni mwa mamia ya tani za misaada ya kuokoa maisha iliyopakiwa kwenye msafara mrefu wa malori yakiwa yamesimama kwenye upande wa Misri wa kivuko cha mpakani ch a Rafah, huku madereva wakisubiri ruksa ya Israel ili waweze kufikia Wapalestina milioni 2.3 waliozingirwa na walionaswa katika mzozo wa vita vinavyoendelea.