Mkimbizi kutoka Sudan: Sikuwa nataka kurejea nchini mwangu Sudan Kusini
Wakati maelfu ya wananchi wakikimbia machafuko nchini Sudan mashirika ya Umoja wa Mataifa nayo yana haha huku na kule kuhakikisha wanatoa usaidizi kwa wakimbizi hao.
Wakati maelfu ya wananchi wakikimbia machafuko nchini Sudan mashirika ya Umoja wa Mataifa nayo yana haha huku na kule kuhakikisha wanatoa usaidizi kwa wakimbizi hao.
Wataalamu 39 wenye uzoefu mkubwa kutoka serikalini, sekta binafsi, teknolojia, mashirika ya kiraia na wanazuoni wamepatiwa jukumu la kusaidia juhudi za Umoja wa Mataifa za kuhakikisha Akili Mnemba au (AI) inatumika kwa maslahi mapana ya binadamu.
Ofisi ya Umoja wa Mataifa jijini Nairobi, Kenya UNON, imekitunuku tuzo kikundi cha kuhifadhi mazingira cha Mikoko Pamoja tuzo ijulikanayo kama Mtu mahiri wa mwaka wa Umoja wa Mataifa au “UN Person of the year”, tuzo inayotolewa kila mwaka kwa kazi nzuri inayofanyika katika jamii.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo amezungumza na waandishi wa Habari hapa kwenye makao makuu ya Umoja huo muda mfupi kabla ya kuanza kwa kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu wanawake na amani na usalama.
Kama usingalikuwepo Umoja wa Mataifa, dunia ingalisambaratika, kila mtu angefanya atakavyo na uonevu ungekuwepo kuanzia ngazi ya familia, ni kauli ya Mwanazuoni Dkt. Kaanaeli Kaale, Mhadhiri Msaidizi katika Chuo Kikuu cha Mt. Augustine, SAUT nchini Tanzania.
Akili mnemba imebadili fani ya sanaa na utamaduni kwa njia ambazo ha ikutarajiwa. Hata hivyo mabadiliko hayo ni ya muda mrefu.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ambaye yuko Cairo Misri amekutana na Waziri wa Mambo ya Nje w anchi hiyo Sameh Shoukry na kisha kuzungumza kwa pamoja na na waandishi wa habari akisema yuko ziarani Mashariki ya Kati kuona misaada ya kibinadamu inayohitajika inawasilishwa kwa wahitaji huko Ukanda wa Gaza kupitia kivuko cha Rafah.
Zaidi ya nusu ya uso wa dunia imeundwa na maji, maji hayo yanatumika kama chakula, nishati na yanasaidia jamii kustawi lakini watu wengi hawana kabisa rasilimali hii adhimu, huku wengine wanayachukulia kawaida.
Chini ya kilomita moja kutoka Gaza, vibao vya kuengeshean chakula, mafuta, maji, na dawa ni miongoni mwa mamia ya tani za misaada ya kuokoa maisha iliyopakiwa kwenye msafara mrefu wa malori yakiwa yamesimama kwenye upande wa Misri wa kivuko cha mpakani ch a Rafah, huku madereva wakisubiri ruksa ya Israel ili waweze kufikia Wapalestina milioni 2.3 waliozingirwa na walionaswa katika mzozo wa vita vinavyoendelea.
Huko Roma, Italia kwenye makao makuu ya shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo, FAO, kumefanyika hafla ya uzinduzi wa maktaba ya kimataifa ya miti na maua kwa lengo la kuhamasisha uelewa juu ya bayonuai na kufanya maeneo ya miji pia kuwa ya kijani zaidi.