Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Sultan Zoori, akiwa kwenye kitimwendo, ni mkimbizi kutoka Afghanistan akiwa na mkewe Zahra Zoori nchini Iran.
UNHCR Video

Ripoti ya WHO yaonesha matokeo duni ya kiafya kwa wakimbizi na wahamiaji  

Ripoti ya kwanza ya kimataifa ya shirika la Umoja wa Mataifa la Afya, WHO kuhusu afya ya wakimbizi na wahamiaji, imeweka wazi kuwa ulimwenguni kote, mamilioni ya wakimbizi na wahamiaji walio katika mazingira hatarishi, kama vile wafanyakazi wahamiaji wasio na ujuzi, wanakabiliwa na matokeo duni ya kiafya kuliko jamii zinazowapokea, hasa pale ambapo hali ya maisha na kazi ni duni, kulingana na ripoti ya kwanza ya Ulimwenguni ya WHO juu ya. afya ya wakimbizi na wahamiaji. 

Prince Emmanuel mkimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC sasa yuko kambini Dzaleka nchini Malawi. yeye ni mpishi mzuri wa chapati lakini vita ya Ukraine na COVID-19 vimesababisha apunguze ukubwa wa chapati.
WFP Video

COVID-19 na Ukraine vimetulazimu tupunguze ukubwa wa chapati- Prince

Athari za kibiashara kutokana na COVID-19 pamoja na vita nchini Ukraine zinaendelea kusambaa duniani na zimebisha hodi hadi kwenye kambi ya wakimbizi ya Dzaleka nchini Malawi ambako ,mkimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC amelazimika kupunguza ukubwa wa chapati ili angalau aweze kuendelea kutoa huduma hiyo pendwa kwa wakimbizi na wakati huo huo apate angalau faida kidodo ili akidhi mahitaji yake na aweze kujitegemea

Sauti
2'42"
Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu watoto kwenye maeneo ya mizozo, Virginia Gamba amewasilisha ripoti ya mwaka ya Katibu Mkuu kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa
UN Photo/Eskinder Debebe

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lajadili ripoti ya mwaka 2021 ya watoto katika maeneo yenye mizozo

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekuwa na mjadala wake wa mwaka kuhusu watoto kwenye maeneo yenye mizozo ambapo Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu watoto hao, Virginia Gamba amewasilisha ripoti ya mwaka ya Katibu Mkuu ambayo iliwekwa bayana kwa umma tarehe 11 mwezi huu wa Julai ikitaja aina sita ya vitendo vibaya zaidi vya ukiukwaji dhidi ya watoto. 

Esperance Tabisha ajulikanaye pia kama Esperanza akiwa nje ya makazi yao mapya huko Ontario Canada na ni kutokana na programu ya mkimbizi kuhamia nchi ya tatu chini ya mkataba wa kimataifa wa wakimbizi wa mwaka 2018.
UN News Video

Esperance Tabisha: Kutoka kuwa mkimbizi Kakuma hadi mbunifu wa mitindo Canada

Esperance Tabisha, raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye sasa ni mnufaika wa mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu wakimbizi, GCR uliopitishwa mwaka 2018 wenye vipengele kadhaa ikiwemo kuhamishia wakimbizi nchi ya tatu. Alikimbia vita DRC na kuingia kambi ya Kakuma nchini Kenya mwaka 2010 na mwaka 2019 akahamia Canada kupitia msaada wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR.