Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mpaka wa Burundi na DR Congo. UNHCR inawasaidia wakimbizi wa Burundi waliokuwa DR Congo kurejea nyumbani.
Screenshot

Waliokuwa wakimbizi nchini DRC wafurahia kurejea nyumbani Burundi  

Raia 272 kutoka familia 78 wa Burundi waliorejea nchini Burundi kutoka kambi ya wakimbizi ya Lusenda katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo mwishoni mwa wiki iliyopita wamekaribishwa na wanachi wenzao, serikali na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi ili waanze maisha katika nchi yao waliyoikimbia kwa vipindi tofauti kutokana na hali mbaya ya usalama 

Katibu Mkuu wa UN António Guterres akihutubua mkutano wa Jukwaa la Kiuchumi duniani.
UN/Eskinder Debebe

Dunia imekosa mshikamano- Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amehutubia mkutano wa Jukwaa la uchumi duniani, WEF na kuwaeleza viongozi wa sekta ya biashara wanaoshiriki kuwa kinachokosekana hivi sasa duniani ni mshikamano wa kimataifa.
 

Katika umri wa miaka 22 tu, Mariama Camara Cire (katikati) ni mwanafunzi, mkulima na pia mwanzilishi wa chama kinachopiga vita unyanyasaji dhidi ya wanawake. Mariama anaungwa mkono na programu ya ITC ambayo ni taasisi tanzu ya Kamati ya Umoja wa Mataifa y
Screenshot/ITC

Camara Mariama Ciré: Mfano wa kuigwa kupitia kwenye kilimo Guinea Conakry 

“Habari, naitwa Camara Mariama Ciré kutoka Guinea Conakry…,” ndivyo anavyoanza Mariama Camara Cire kwa kujitambulisha kuwa anatokea Guinea Conakry moja ya nchi za Afrika Magharibi inayopakana na Bahari ya Atlantiki katika upande wake wa Magharibi na kwingine ikipakana na Guinea Bissau, Sierra Leone, Côte d'Ivoire, Senegal na Mali.