UNSMIL ya Libya yaongezewa miezi mitatu zaidi
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo kwa kauli moja limepitisha azimio la kuongeza muda wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa usaidizi nchini Libya, UNSMIL hadi tarehe 30 mwezi huu wa Aprili.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo kwa kauli moja limepitisha azimio la kuongeza muda wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa usaidizi nchini Libya, UNSMIL hadi tarehe 30 mwezi huu wa Aprili.
Raia 272 kutoka familia 78 wa Burundi waliorejea nchini Burundi kutoka kambi ya wakimbizi ya Lusenda katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo mwishoni mwa wiki iliyopita wamekaribishwa na wanachi wenzao, serikali na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi ili waanze maisha katika nchi yao waliyoikimbia kwa vipindi tofauti kutokana na hali mbaya ya usalama
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amewatumia ujumbe wa heri ya mwaka mpya wakichina wananchi wa China ambao wanasherekea mwaka wa Simba Marara
Janga la COVID-19 limethibitisha bayana ukosefu wa usawa uliopo ulimwenguni leo ambapo nchi zilizoendelea shule zilifungwa lakini watoto waliendelea na masomo kwa njia ya mtandao wakati wanafunzi katika nchi zinazoendelea, shule zilifungwa, na watoto hawakujifunza kabisa.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amehutubia mkutano wa Jukwaa la uchumi duniani, WEF na kuwaeleza viongozi wa sekta ya biashara wanaoshiriki kuwa kinachokosekana hivi sasa duniani ni mshikamano wa kimataifa.
“Habari, naitwa Camara Mariama Ciré kutoka Guinea Conakry…,” ndivyo anavyoanza Mariama Camara Cire kwa kujitambulisha kuwa anatokea Guinea Conakry moja ya nchi za Afrika Magharibi inayopakana na Bahari ya Atlantiki katika upande wake wa Magharibi na kwingine ikipakana na Guinea Bissau, Sierra Leone, Côte d'Ivoire, Senegal na Mali.