Hapa na Pale
Baraza la Usalama limepitisha, Alkhamisi asubuhi, azimio liloruhusu kuongeza, kwa muda, vikosi vya wanajeshi wa MONUC ili kudhibiti vurugu na fukuto la mapigano yaliozuka kwenye eneo la mashariki, katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo. Mapigano katika eneo hilo la nchi yalisababisha raia 250,000 kung’olewa makazi katika miezi ya karibuni, umma ambao unategemea misaada ya dharura kutoka mashirika ya kimataifa ili kukidhi mahitaji ya kimsingi. Azimio limependekeza kupelekwe wanajeshi wa kimataifa 2,785 pamoja na vikosi vya askari polisi 300. ~