Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mapigano yawanyima wanafunzi 150,000 fursa ya kuilimishwa katika JKK: UNICEF

Mapigano yawanyima wanafunzi 150,000 fursa ya kuilimishwa katika JKK: UNICEF

Veronique Taveau, Msemaji wa Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF) aliwaambia waandishi habari wa kimataifa Geneva, ya kwamba kutokana na mapigano yaliotanda katika JKK, skuli kadha zimelazimika kufungwa katika eneo la Rutshuru, na ambayo wanafunzi 150,000 ziada wananyimwa fursa ya masomo, maana hali ni ya wahka mkubwa na ya hatari sana.