Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkariri wa masuala ya ubaguzi ashtumu mashambulio ya wageni Afrika Kusini

Mkariri wa masuala ya ubaguzi ashtumu mashambulio ya wageni Afrika Kusini

Doudou Dienne, Mkariri Maalumu wa UM anayehusika na masuala ya ukabila, ubaguzi wa rangi wa kisasa, chuki za wageni wa nchi na utovu wa ustahamilivu, leo amewasilisha taarifa maalumu yenye kuelezea huzuni alionayo kuhusu kiwango kilichofurutu ada cha yale mashambulio ya chuki yaliofanyika Afrika Kusini karibuni, dhidi ya wahamiaji wa mataifa jirani, na pia dhidi ya kundi la makabila madogo ya wahamiaji yaliopo nchini, hujuma ambazo alisema ziliendelezwa mjini Johannesburg na vile vile kwenye vitongoji jirani, na kusababisha mauaji ya watu zaidi ya 40 na majeruhi kadha.