Mkutano wa ngazi za juu kuitishwa Makao Makuu kuzingatia Darfur
Ijumaa, Septemba 21, kulifanyika kikao cha faragha kwenye Makao Makuu na kuhuduriwa na wawakilishi kutoka mataifa 26, ikiwemo Sudan, na pia wajumbe wa kudumu wa Baraza la Usalama, wawakilishi wa mataifa jirani na Sudan, na wawakilishi wa Baraza la Usalama na Amani la Umoja wa Afrika (AU) pamoja na maofisa wa Umoja wa Ulaya, na wawakilishi wa kutoka Umoja wa Nchi za Kiarabu, halkadhalika.