Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Haki za binadamu zinaendelea kuharamishwa Sudan

Haki za binadamu zinaendelea kuharamishwa Sudan

Mkariri Maalumu juu ya Haki za Kiutu katika Sudan, Sima Samar katika risala yake mbele ya wajumbe wa kikao cha Baraza la UM juu ya Haki za Kiutu, ambacho kinakutana mjini Geneva, hivi sasa, alionya kwamba vikosi vya Serekali ya Sudan, pamoja na wanamgambo kadhaa, wakijumuika na makundi ya waasi na vile vile vikundi vya wapinzani kutoka taifa jirani la Chad bado wanaendelea kuharamisha haki za binadamu katika Sudan. Alisema imethibitika makundi hayo huendeleza, kihorera, mauaji ya watu ndani ya Sudan bila kujali adhabu, hususan katika jimbo la Darfur.