Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahakama ya ICTR na wanadiplomasiya washauriana na Kenya utaratibu wa kumshika mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki

Mahakama ya ICTR na wanadiplomasiya washauriana na Kenya utaratibu wa kumshika mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki

Hassan Bubacar Jallow, Mwendesha Mashitaka wa Mahakama ya UM juu ya Rwanda (ICTR)amefanya mazungumzo mjini Nairobi na wawakilishi wa ofisi za ubalozi 25 pamoja na mawaziri wa Kenya, akiwemo Waziri wa Sheria, Martha Karua kuzingatia juhudi za pamoja za kumshika yule mfanya biashara mtoro wa Rwanda, Felicien Kabuga ambaye alituhumiwa kufadhilia msaada wa kuendeleza mauaji ya halaiki nchini mnamo mwaka 1994.