Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jumuiya ya kimataifa kuongeza muda wa UNMEE

Jumuiya ya kimataifa kuongeza muda wa UNMEE

Azzouz Ennifar, Mwakilishi wa Muda wa KM kwa Ethiopia na Eritrea amewasilisha, hivi karibuni, ripoti inayosisitiza kwamba itakuwa ni jambo la busara kuu ikiwa jumuiya ya kimataifa itakubali kuongeza muda wa kazi za Shirika la UM linalosimamia Huduma za Amani Mipakani kati ya Ethiopia na Eritrea (UNMEE) kwa miezi sita ziada. Ennifar alibashiria hatari ya kufumka tena maafa na vurugu katika eneo hilo la mipakani UM ukishindwa “kukwamua mzoroto wa mazungumzo ya upatanishi” kati ya Ethiopia na Eritrea.