Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Dkt. Bonifasi Masawe,  akiwaonyesha hatua kwa hatua washiriki, ripoti ya utafiti ulio fanywa wa upimaji udongo.
UN News/John Kabambala

FAO Tanzania na Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine wapima udongo katika wilaya 6 Tanzania

Kilimo ni nguzo muhimu ya uchumi na chanzo kikuu cha chakula. Kupata mazao bora na mavuno mengi kunategemea sana ubora wa udongo. Hatua hizi zikichukuliwa kila pembe ya dunia kutasaidia wakulima kuelewa mchanganyiko wa madini na virutubisho katika udongo wao, linaelimisha shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO.

Sauti
5'59"
Hayat, mkulima na mfugaji akiwa na mbuzi wake huko shambani mwake Badham nchini Somalia.
FAO/Arete/Isak Amin.

Ufugaji endelevu unaonufaisha jamii bila kuharibu mazingira wamulikwa huko Roma, Italia

Mkutano wa kwanza kabisa wa kimataifa kuhusu marekebisho ya mfumo wa ufugaji wa Wanyama umeanza hii leo kwenye makao makuu ya shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo, FAO lengo likiwa ni kusaka mbinu za kuwezesha ufugaji huo uwe na mnepo zaidi, usiharibu mazingira na uchangie katika maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii, halikadhalika sayari yenye afya.

Sauti
3'5"
Waziri wa Afya wa Kenya Susan Nakhumicha Wafula.
UN News

Kama COVID-19 ilivyotiliwa mkazo ifanyike hivyo kwa Kifua Kikuu

Mkutano wa ngazi ya juu kuhusu mapambano dhidi ya kifua kikuu au TB ukifanyika leo hapa katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani, Waziri wa Afya wa Kenya Susan Nakhumicha Wafula amesema kutokomeza TB ifikapo mwaka 2030 inawezekana endapo Dunia itashikama na kuweka msokumo mkubwa kwa ugonjwa huo kama ilivyofanya wakati wa mlipuko wa janga la COVID-19.

Audio Duration
2'7"
Madina Jubilate Kimaro, Balozi wa Mazingira wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto duniani, UNICEF nchini Tanzania.
UN/Assumpta Massoi

Samadi ya ng’ombe yachukua nafasi ya mkaa wa miti - Madina

Je umewahi kuona changamoto ukaigeuza fursa si kwako tu bali kwa wengine pia? Hiyo imemtokea Madina Jubilate Kimaro, msichana mwenye umri wa miaka 19 nchini Tanzania ambaye akiwa kwa bibi au nyanya yake jijini Dar es salaam nchini humo aliwaza na kuwazua kuona ni kwa vipi anaweza kutumia samadi ya ng’ombe kuwa bidhaa ya kusaidia kukabili mabadiliko ya tabianchi.

Sauti
6'24"
Wasichana wa baraza la ushauri la vijana, Nairobi wakitazama app ya OKY.
UNICEF Kenya

Apu ya OKY na hedhi salama yasongesha SDG 3- UNICEF

Shirika la umoja wa mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, limezindua apu maalum ya wasichana kufuatilia maelezo wakati wa hedhi. Apu hiyo ni mahsusi kwa wasichana wa mataifa yanayoinukia na yaliyo masikini. Apu hii inaleta matumaini wakati huu ambapo viongozi wa dunia wanakutana New York, Marekani kutathmini maendeleo ya malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. 

Sauti
2'47"