Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Msichana mwenye umri wa miaka kumi alitoroka nyumbani baada ya kugundua familia yake ilipanga kumfunza kama ngariba wa ukeketaji/C. Kwa sasa anaishi katika nyumba salama ya UNICEF huko Port Loko, Sierra Leone, na anahudhuria shule.
© UNICEF/Olivier Asselin

Wanaume na wavulana jitokezeni mtokomeze FGM

Hii leo ni ikiwa ni siku ya kimataifa ya kutokomeza ukeketaji wa wanawake na wasichana ,Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametaka wanaume na wavulana wapaze sauti zao kusaidia kutokomeza mila hiyo potofu na hatarishi.  

Sauti
2'10"
Mtoto akitabasamu darasani wakati wa ziara ya pamoja ya ECW na Norway kwenye maeneo nufaika ya miradi ya elimu inayofadhiliwa na pande mbili hizo.
ECW

Watoto milioni 222 walio katika maeneo yaliyoathirika na migogoro wanahitaji msaada wa haraka wa elimu:ECW 

Mfuko wa Umoja wa Mataifa unaohusika na kusongesha elimu kwenye maeneo yenye majanga na mizozo ya muda mrefu, Education Cannot Wait, ECW au kwa lugha ya Kiswahili, Elimu Haiwezi Kusubiri, pamoja na wadau wamesisitiza umuhimu wa kusaidia mamilioni ya watoto walio katika mazingira ya migogoro ili waweze kupata elimu, wakisema elimu ndio ufunguo wa kuwakomboa watoto hao hususan wasichana katika maisha yao ya siku za usoni.

Sauti
3'7"
Watu walioyakimbia makazi yao katika eneo la Equatoria Magharibi Sudan Kusini wakikutana na viongozi wa vijiji.
UNMISS

Maelfu ya wakimbizi wa ndani wa Tambura warejea makwao

Sudan Kusini ni moja ya nchi iliyoathirika kwa muda mrefu na vita vya wenyewe kwa wenyewe ambapo mara kwa mara makundi ya wapiganaji wenye silaha yalikuwa yakivamia katika vijiji na kuwaua raia na kupora mali zao. Kutokana na sababu hiyo wananchi wengi wamekuwa wakikimbilia katika kambi za kijeshi zilizoko karibu na maeneo yao ili kusaka hifadhi.

Sauti
4'9"