Wahisani wafanikisha kutenganishwa kwa watoto mapacha
Mapacha wawili waliozaliwa huko Sana’a nchini Yemen wakiwa wameungana kuanzia kifuani hadi tumboni hatimaye wametenganishwa huko Jordan na wamerejea nyumbani.
Mapacha wawili waliozaliwa huko Sana’a nchini Yemen wakiwa wameungana kuanzia kifuani hadi tumboni hatimaye wametenganishwa huko Jordan na wamerejea nyumbani.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF linaendesha program maalum ya lishe kwenye kaunti ya Garissa nchini Kenya kwa lengo la kunusuru maisha ya mamia ya watoto wanaosumbuliwa na utapiamlo.
Ujumbe wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS umefanya ziara na viongozi wa dini kuwatembelea wakimbizi wa ndani walioko Nagero huko Tambura li kuweza kuwajengea matumaini lakini pia kusikiliza mahitaji yao.
Idadi ya watu wenye njaa barani Afrika inaendelea kuongezeka, ikichochewa na uwepo wa migogoro, mabadiliko ya tabianchi na kuzorota kwa uchumi sababu nyingine mbalimbali ikiwemo pia janga la COVID-19. Imesema ripoti iliyotolewa leo na viongozi wa mashirika matatu ya kikanda barani Afrika ambayo yametoa wito wa kuchukua hatua zaidi juu ya mabadiliko ya mifumo ya kilimo.
Ushirikiano kati ya vyombo vya usalama ikiwemo polisi na FRDC ambalo ni Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na vikosi vya walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanaohudumu chini ya Mwavuli wa MONUSCO, umeendelea kuzaa matunda kwa kuwahakikishia usalama wananchi wa maeneo ya mashariki mwa DRC.
Wakimbizi 11,000 kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC waliokimbilia nchi jirani ya Uganda hivi karibuni kufuatia machafuko yanayoendelea Mashariki mwa DRC wameanza kurejea nyumbani kwa hiyari na kilichowasukuma ni usemi wa wahenga kuwa nyumbani ni nyumbani.
Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa mazingira duniani, UNEP wiki hii Jumanne ya tarehe 07 limewatangaza washindi wanne wa tuzo yake ya juu kabisa ya mazingira ijulikanayo kama “champions of the Earth Award” kwa mwaka 2021. Mabingwa hao walichaguliwa kutokana na mchango katika mazingira na uongozi wao katika kuendeleza hatua za ujasiri na madhubuti kwa niaba ya watu wengine wa sayari dunia. Dk Gladys Kalema-Zikusoka wa Uganda ni mmoja wa tuzo hiyo ya UNEP katika kipengele cha Sayansi na Ubunifu.
Siku kama ya leo tarehe 9 mwezi Desemba mwaka 1961, iliyokuwa Tanganyika au Tanzania Bara ilipata Uhuru wake kupitia mchakato uliosimamiwa na Umoja wa Mataifa. Siku 5 baadaye, nchi hiyo huru ilijiunga na Umoja wa Mataifa na kuwa mwanachama hadi leo na hii leo inaposherehekea miaka 60 ya uhuru wake, pia inatambua faida inazozipata kwa kuwa mwanachama wa UN kama anavyoeleza Kaimu Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Songelael Shilla alipozungumza na Idhaa hii jijini New York Marekani.
Machafuko yanayoendelea katika jimbo la Darfur nchini Sudan yamewasababisha maelfu ya watu kufungasha virago na kuyakimbia makazi yao tangu mwezi Novemba mwaka huu, wengi wakitawanywa ndani ya nchi na wengine kwenye mpaka wa nchi Jirani ya Chad limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na kuongeza kuwa linatiwa hofu kubwa na hali hiyo.
Ripoti mpya iliyotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF imesema janga la COVID-19 limeleta hali mbaya zaidi kwa watoto kuwahi kushuhudiwa katika historia yake ya miaka 75 nakuzitaka nchi kuongeza juhudi kuwanusuru watoto.