Tusipoteze muda na wasioamini kwenye mabadiliko ya tabianchi- Tanzania
Mjadala Mkuu wa mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74, ukiingia siku ya nne hii leo kwenye makao makuu ya umoja huo jijini New York, Marekani, Tanzania imesema imetenga asilimia 32 ya eneo la nchi kama hifadhi ya misitu kama njia mojawapo ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.