WFP na Impact Hub Kigali wazindua mpango wa kusaidia uvumbuzi wa mfumo wa chakula nchini Rwanda
Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP na taasisi ya Impact Hub Kigali, IHK ya nchini Rwanda pamoja na wadau wengine kama USAID (BHA) na Wizara ya Mambo ya Nje ya Denmark, wamezindua shindano la Mifumo ya Chakula nchini Rwanda walilolipa jina IGNITE kwa lengo la kukuza utatuzi wa ndani ya nchi ili kukabiliana na changamoto za mifumo ya chakula. Mpango huo utatoa usaidizi wa kiufundi na jumla ya dola 300,000 za usaidizi wa kifedha.