Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mkulima wa Rwanda akiwa ameshika maharage mkononi baada ya mavuno
© WFP/Fredrik Lerneryd

WFP na Impact Hub Kigali wazindua mpango wa kusaidia uvumbuzi wa mfumo wa chakula nchini Rwanda 

Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP na taasisi ya Impact Hub Kigali, IHK ya nchini Rwanda pamoja na wadau wengine kama USAID (BHA) na Wizara ya Mambo ya Nje ya Denmark, wamezindua shindano la Mifumo ya Chakula nchini Rwanda walilolipa jina IGNITE kwa lengo la kukuza utatuzi wa ndani ya nchi ili kukabiliana na changamoto za mifumo ya chakula. Mpango huo utatoa usaidizi wa kiufundi na jumla ya dola 300,000 za usaidizi wa kifedha. 

Walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu kwenye ujumbe wa MINUSCA nchini CAR wakiwa ziarani kwenye gereza huko Berberati.
TANBAT5/Kapteni Asia Hussein

TANBAT-5 waanza mwaka mpya kwa kutembelea gereza CAR na kutoa msaada

Nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, kikosi cha 5 cha Tanzania, TANBAT-5 kinachohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MINUSCA kimefungua mwaka 2022 kwa kutembelea gereza la wafungwa lililoko wilaya ya Berberati, mkoa wa Mambere Kadei, eneo ambalo ni makao makuu ya kikosi hicho, ikiwa ni kitendo cha ukarimu kwa wafungwa hao. 

Sauti
2'17"
Mhudumu wa afya akimpatia chanjo dhidi ya COVID-19 mkazi wa wilaya ya Kasungo nchini Malawi.
© UNICEF/ Thoko Chikondi

Chanjo chanjo chanjo ndio jawabu mujarabu dhidi ya Omnicron- WHO

Virusi aina ya Omnicron vikiendelea kuwa sababu ya kasi kubwa ya maambukizi ya ugonjwa wa Corona au COVID-19 hivi sasa duniani kote, shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO hii leo limesema ni muhimu hatua zaidi zikachukuliwa ili kusaidia nchi zote kupata haraka iwezekanavyo chanjo dhidi ya Corona kwa kuwa ndio mkombozi iwapo mtu anaambukizwa na tayari ana chanjo. 

Sauti
2'39"