Walinda amani kutoka Tanzania watunukiwa sarafu ya ujasiri na utendaji mzuri
Walinda amani wanne wa Umoja wa Mataifa kutoka nchini Tanzania wanaohudumu nchini Jamhuri ya Kati wametunukiwa sarafu ya ujasiri na utendaji kazi mzuri.
Walinda amani wanne wa Umoja wa Mataifa kutoka nchini Tanzania wanaohudumu nchini Jamhuri ya Kati wametunukiwa sarafu ya ujasiri na utendaji kazi mzuri.
Wiki tatu baada ya kimbunga Odette kinachofahamika kimataifa kwa jina Rai kuharibu eneo kubwa la nchi ya Ufilipino, Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP kupitia taarifa yake iliyotolewa hii leo katika mji mkuu wa nchi hiyo, Manila, limeonya kwamba lishe na uhakika wa chakula viko hatarini katika jamii zilizo katika maeneo yenye hali ngumu ikiwa mahitaji ya haraka ya chakula hayatawafikia katika kipindi cha miezi sita ijayo.
“Jina langu ni Zulaikha Patel.” Huyo ni Zulaikha Patel. Msichana mwenye umri wa miaka 19 hivi sasa. Raia wa Afrika Kusini.
Utafiti mpya uliofanywa na wanasayansi wa shirika la kimataifa la utafiti wa saratani, IARC na wale kutoka Kenya, Tanzania na Malawi umebaini pombe kuwa kinywaji hatarishi na kichocheo cha saratani ya tumbo, ESCC, hususan miongoni mwa wanaume.
“Kutokana na kuenea kwa mnyumbuliko mpya wa omicron katika maeneo yote duniani, maambukizi mapya yalifikia milioni 9.5 na vifo vilizidi 41,000 ulimwenguni kuanzia Desemba 27 hadi Januari 2. "Na tunajua kwamba namba hizi ziko chini ya zile halisi." Anaonya Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Afya la Umoja wa Mataifa, Dkt Tedros Ghebreyesus akitoa wito kwa mara nyingine tena kwa usambazaji sawa wa chanjo dhidi ya virusi vya corona.
Mkopo uliotolewa na mfuko wa Umoja wa Mataifa wa maendeleo ya kilimo duniani IFAD nchini Misri umekuwa na manufaa makubwa kwa wakulima wadogo na kutengeneza maelfu ya ajira mpya hali iliyofanya mpaka Bodi tendaji ya IFAD kufunga safari mpaka nchini humo kujionea wenyewe. Anold Kayanda anakuletea taarifa kutoka kwa wakulima wadogo wakieleza namna maisha yao yalivyobadilika. Taarifa ya Anold Kayanda inaeleza zaidi.
Waandishi wa habari 55 waliuawa katika mwaka uliopita, 2021, uchunguzi wa shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu na Utamaduni, UNESCO umeeleza.
Ikiwa mwezi huu wa Januari ni mwezi wa kuelimisha kuhusu saratani ya shingo ya kizazi, Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani, WHO Dkt. Tedros Ghebreyesus amesema saratani hiyo inaweza kuwa ina ya kwanza ya saratani kutokomezwa ulimwenguni iwapo serikali itaongeza huduma za tiba na kinga.
Nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kuweka utulivu MINUSCA umefadhili ukarabati wa dampo la kutupia taka kwenye mji mkuu Bangui kama njia ya kulinda mazingira sambamba na kuboresha maisha ya wakazi wanaozunguka dambo hilo.
Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu sayansi na utamaduni UNESCO, limelaani mauaji ya mwandishi wa habari Sai Win Aung, anayejulikana pia kama A Sai K, nchini Myanmar yaliyotokea Desemba 25, 2021 nchini Myanmar, karibu na mpaka na Thailand.