Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Watoto wakichota maji kwenye bomba kambini Bulengo jimboni Kivu Kaskazini nchiniDRC.
UN News/Byobe Malenga

Hatua zichukuliwe kuondoa madanguro kwenye kambi za wakimbizi- UN

Kufuatia kuwepo kwa ripoti za ubakaji na biashara ya ngono kwenye kambi za wakimbizi wa ndani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Naibu Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini humo ambaye pia ni Mratibu wa masuala ya kibinadamu Bruno Lemarquis ameongoza ujumbe wa mabalozi kutoka nchi za nje kwenye ziara katika moja ya kambi hizo huko Kivu Kaskazini kukutana na wakimbizi. Shuhuda wetu ni Byobe Malenga, mwandishi wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa nchini DRC. 

Regine Ngamanene Okando (kushoto), mwandishi wa habari wa Radio Canal Rafiki kwenye mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini na Erickson Luhembwe, mwandishi wa habari wa RFI katika majimbo ya Ituri na Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC…
UN News/George Musubao

Wanahabari tukikatishwa tamaa tunawaangusha wananchi – Waandishi wa habari DRC

Hii leo ikiwa ni siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari duniani maudhui yakiwa Kuumba mustakabali wa Haki: Uhuru wa kujieleza kama kichocheo cha haki zote za binadamu, huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC mapigano ya mara kwa mara yamekwamisha harakati za waandishi wa habari kupatia wananchi haki yao ya msingi ya kupata habari.

Sauti
6'28"
Jamii la kabila la watu wa asili ambao wanaishi kwenye misitu iliyo ndani zaidi katika ukingo wa Mto Congo nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC.
UNICEF/Vincent Tremeau

Miti ya migunga yarejesha matumaini kwa wakazi wa msitu wa Congo

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, mradi unaofadhiliwa na Benki ya Dunia wa kupanda miti aina ya migunga imeondoa tishio la ukataji miti holela kwenye msitu wa bonde la mto Congo, ambao ni wa pili kwa ukubwa duniani katika kufyonza hewa ya ukaa na sasa wananchi wananufaika sio tu kwa kupata mkaa bali pia hata watu wa jamii ya asili wanaweza kupata kitoweo porini.

Sauti
2'16"
Wakati wa siku ya afya duniani 7 Aprili 2023, walinda amani wa UN kutoka kikosi cha Tanzania cha kutoa msaada wa haraka, TANZQRF katika kwneye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani, MONUSCO nchini DRC  wametoa huduma za kupima magonjwa yasiyo ya ku…
TANZQRF3/Methew Makoba

Siku ya Afya Duniani: Walinda amani wa UN kutoka TZ nchini DRC waadhimisha kwa vitendo

Leo ni siku ya afya duniani ujumbe ukiwa ni Afya kwa Wote ambapo walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO, wametumia siku hii kuwapima magonjwa yasiyo ya kuambukiza, NCDs, wakazi wa Beni-Mavivi jimboni Kivu.

Sauti
4'41"
Mkazi huyu wa Beni, jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC aitwaye Joel Methya Ndeku alipoteza ndugu zake katika mauaji ya mwaka 2018 na hadi leo hafahamu chochote kuhusu wauaji.
UN News/George Musubao

UN itusaidie tupate ukweli na haki kwa kuuawa kwa ndugu zetu – Mkazi Beni, DRC

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC mashambulizi yanayoendelea mashariki mwa nchi hiyo kwenye jimbo la Kivu Kaskazini yanasababisha sio tu vifo bali machungu yasiyoisha kwa familia za waliouawa kwa kushindwa kufahamu ukweli wa nini kiliwafika jamaa zao, nani aliwaua, na haki gani imetendeka na sheria dhidi ya waliohusika. 

Sauti
4'16"
Sostine ambaye ni mchuuzi wa maji katika mji wa Goma jimboni Kivu Kaskazini nchini DRC anamweleza mwanahabari mtoto Liesse ya kuwa hulazimika kuweka dawa kwenye madumu ya maji kwa sababu maji ya Ziwa Kivu yana taka.
UNICEF VIDEO

UNICEF yawezesha wanahabari watoto kupasha umma kuhusu changamoto za maji DRC

Hii leo ni siku ya maji duniani na ninakupeleka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako huko mtoto Liesse mwenye umri wa miaka 17 amefuatilia upatikanaji wa maji safi ya kunywa kwenye eneo la Goma jimboni Kivu Kaskaizini baada ya kupatiwa mafunzo ya uandishi wa habari na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto duniani, UNICEF na hatimaye taarifa yake kutangazwa na Radio Okapi ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo

Sauti
2'23"
Ndoto ya Thérèse (pichani) ni kuwa Gavana wa jimbo la Tanganyika. Hapa ni katika darasa jipya lililojengwa kwenye shule ya msingi ya Lubile jimboni Tanganyika kwa msaada wa UNICEF na Education Cannot Wait.
© UNICEF/Josue Mulala

UNICEF na ECW yarejesha matumaini kwa watoto waiotumikishwa vitani DRC

Mradi mpya wa shule  nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC uliozinduliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto,  UNICEF na wadau wake kwa ufadhili kutoka mfuko wa Umoja wa Mataifa wa kuchagiza elimu kwenye maeneo ya mizozo, Education Cannot Wait, ECW, au Elimu Haiwezi Kusubiri umewezesha watoto waliokuwa wametumikishwa vitani kuanza kurejea kwenye masomo na hata kutangamana na wenzao kwa amani.  

Sauti
2'45"