Wakimbizi wajumuishwa vyema kule walikokimbilia
Siku ya kimataifa ya wakimbizi duniani imeadhimishwa duniani kote tarehe 20 mwezi huu wa Juni. Maadhimisho haya yanafanyika wakati hivi sasa kuna zaidi ya watu milioni 80 duniani kote ambao wamelazimika kukimbia makazi yao kutokana na vita, ghasia na mateso na hivyo kujikuta wameacha kila kitu.