Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

DR Congo

Francine na watoto wake watatu walilazimika kuondoka kijijini kwake kutokana na mzozo usiokoma mashariki mwa DRC. Sasa wanapokea msaada wa WFP katika kambi ya wakimbizi wa ndani huko Kivu Kaskazini.
© WFP/Michael Castofas

WFP DRC waomba msaada wa $Mil 425 kusaidia wakimbizi wa ndani

Wakati Mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemorkasia Kongo DRC ikiripoti kuwa na zaidi ya wakimbizi wa ndani 738,000 kwa kipindi cha mwaka huu wa 2024 pekee kutokana na kuongezeka kwa machafuko, Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP limeeleza kuwa na uhitaji wa haraka wa dola milioni 425 ili waweze kuwasaidia wakimbizi hao wanaoongezeka kila uchao. 

Sauti
1'49"
Mariam Suleiman, Mkimbizi kutoka DR Congo anayeishi katika makazi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya.
UNHCR Video

Wanawake tuna ujuzi, tuna uwezo na tunaweza: Mariam Suleiman

Mwanamke akiwezeshwa anaweza, huo ndio umekuwa usemi wa Umoja wa Mataifa ukipigia chepuo wanawake kujumishwa katika kila Nyanja ya Maisha ili waweze kujikwamua kiuchumi na kuchangia katika maendeleo ya jamii. Usemi huo unaungwa mkono na mwanamke mkimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC ambaye sasa anaishi Kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya.

Sauti
2'7"
Hapa ni Beni, jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Brazil wanaohudumu kikosi cha kujibu mashambulizi FIB cha MONUSCO wakipatia mafunzo wanajeshi 30 kutoka jeshi la serikali, FARDC j…
MONUSCO/Ado Abdou

DRC: MONUSCO yapatia wanajeshi 30 wa FARDC mbinu za kukabili waasi msituni

Siku zikizidi kuhesabiwa kwa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO, kuondoka nchini humo, ujumbe huo unaendelea kutekeleza wajibu wake wa kujengea uwezo jeshi la serikali, FARDC kuweza kukabili vikundi vilivyojihami ambavyo vinatajwa kuhusika na asilimia 65 ya matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu nchini humo mwezi Februari mwaka huu, kwa mujibu wa ripoti ya pamoja ya Umoja wa Mataifa na serikali. 

Sauti
2'12"
Innoss B(kushoto) na Mkurugenzi wa WFP DRC, Peter Musoko(Kulia). Innoss B akitia saini barua rasmi ya kuteuliwa kama Msaidizi wa Ngazi ya Juu wa WFP nchini DRC, akihimiza milo yenye afya na lishe bora.
© WFP/Charly Kasereka

Innoss’B kutumia muziki kusongesha elimu na lishe bora DRC

Nimeshuhudia njaa mara nyingi sana wakati wa utoto wangu, kabla ya kwenda shule tulikuwa na njaa na kabla ya kulala tulikuwa na njaa, ndivyo asemavyo mwanamuziki Innocent Balume, al maaruf Innoss’B ambaye ametangazwa kuwa muungaji mkono wa ngazi ya juu wa shirika la  Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP katika kusongesha milo yenye afya na lishe bora nchini mwake Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Sauti
2'6"
Kamanda wa TANZBATT-10, Luteni Kanali John Peter Kalabaka akimkabidhi bendera ya Tanzania Luteni Kanali  Vedasto Ernest Kikoti ikiwa ni ishara ya kukabidhiana majukumu ya ulinzi wa amani huko Beni Mavivi jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokra…
TANZBATT-10

Wananchi DRC eleweni na ikubalini dhamira ya UN ya kulinda raia - TANZBATT-11

Hii leo huko jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kikosi cha 10 cha Tanzania (TANZBATT-10)  kilichoko kwenye brigedi ya mapigano (FIB) ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO imekabidhi majukumu kwa kikosi cha 11, TANZBATT-11, katika hafla iliyofanyika eneo la Beni-Mavivi. Msimulizi wetu ni Kapteni Abubakari Muna, Afisa Habari wa TANZBATT-10.

Sauti
3'28"