Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

DR Congo

Uzinduzi wa mpango wa kusaidia askari wa zamani wa msituni na vijana walio kwenye mazingira hatarishi ili waweze kujipatia kipato. Hapa ni Nyiragongo, jimboni Kivu Kaskazini na mradi unatekelezwa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani DRC, MONUSCO
MONUSCO/Michael Ali

MONUSCO na COMOA washirikiana kuimarisha usalama Goma, DRC

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani MONUSCO kupitia kitengo chake cha kupokonya silaha askari waliojisalimisha, kuvunja makundi na kujumuisha askari hao katika jamii, DDR umepatia shirika la kiraia liitwalo COMOA, takribani dola 50,000 ili kufunga taa 60 za sola kwenye kitongoji cha Karuba kilichoko takribani kilometa 50 kutoka mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini, Goma.

 

Sauti
2'38"
Maji safi ya kunywa
World Bank/Arne Hoel

Mradi wa maji wadhibiti kipindupindu DRC 

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF kwa ushirikiano na kituo cha kimarekani cha kudhibiti magonjwa, CDC wamesaidia ujenzi wa tenki za maji kwa ajili ya wakazi wa Kiziba mjini Goma, jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na hivyo kusaidia kuepusha maambukizi ya magonjwa yatokanayo na matumizi ya  maji machafu. 

Sauti
2'9"
Akarurimana James ni mkimbizi kutoka Burundi ambaye amenufaika na ardhi iliyotolewa na serikali ya DRC kwa ajili ya wakimbizi na wenyeji wao kwa lengo la kuimarisha kujitegemea.
UN/Byobe Malenga

Wakimbizi wa Burundi nchini DRC washukuru kupatiwa ardhi ya kilimo

Nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC, serikali imetangaza kutenga ekari  500 za ardhi kwa ajili ya kilimo itakayotumiwa na wakimbizi kutoka Burundi pamoja na wenyeji, kwa lengo la kuimarisha hali ya kujitegemea na kuishi pamoja kwa amani. Kwa kiasi kikubwa wakimbizi hao wamekuwa wakitegemea msaada kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na jamii za wenyeji zinazowahifadhi wakimbizi hao.  

Sauti
2'12"
Mlinda amani kutoka Timu ya kuwahusisha wanawake ya MONUSCO akisambaza barakoa katika kijiji cha Walungu nchini DR Congo
MONUSCO

DNA za walinda amani wa Afrika Kusini huko DRC zakusanywa kubaini baba za watoto 

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, jeshi la Afrika Kusini limepeleka timu yake kwenye  ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MONUSCO,ili kuchunguza vijinasaba vya watoto na wanawake waliobakwa na walinda amani ili hatimaye kuthibitisha iwapo watuhumiwa ni walinda amani kutoka Afrika Kusini na kisha watoto hao watambue baba zao na pia kupatiwa malezi. 

Sauti
2'39"