Uhamasishaji wa nyumba kwa nyumba DRC wachochea watu kupata chanjo ya COVID-19
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF huko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC linatumia wafanyakazi wa kijamii kuhamasisha wakazi wa vitongoji vya mji mkuu, Kinshasa kupata chanjo dhidi ya ugonjwa wa Corona, au COVID-19 kwa kuwa baadhi ya watu bado wanasuasua kupatiwa chanjo hiyo.