Lengo letu ni kuhakikisha kila mtu Afrika anakijua na kukizungumza Kiswahili-Wadau
Maadhimisho ya pili ya siku ya lugha ya Kiswahili duniani yamewadia ni wiki ijayo tarehe 7 ya mwezi Julai ambapo wadau wote wa kiswahili duniani kuanzia kwenye shirika la Umoja wa Mataifa la elimu sayansi na utamaduni UNESCO, kwenye Mataifa wazungumzaji wa lugha hii adhimu hadi ughaibuni mambo yatakuwa bambam, lakini hapa kwenye makao makuu ya umoja wa Mataifa maandalizi yamefikia wapi? Na nini kitajiri? Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa imewaalika wadau wa Kiswahili hapa kwenye makao makuu kufahamu maandalizi yanaendeleaje.