Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Wadau wa lugha ya Kiswahili wakizungumza na Flora Nducha hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa, New York Marekani.
UN News

Lengo letu ni kuhakikisha kila mtu Afrika anakijua na kukizungumza Kiswahili-Wadau

Maadhimisho ya pili ya siku ya lugha ya Kiswahili duniani yamewadia ni wiki ijayo tarehe 7 ya mwezi Julai ambapo wadau wote wa kiswahili duniani kuanzia kwenye shirika la Umoja wa Mataifa la elimu sayansi na utamaduni UNESCO, kwenye Mataifa wazungumzaji wa lugha hii adhimu hadi ughaibuni mambo yatakuwa bambam, lakini hapa kwenye makao makuu ya umoja wa Mataifa maandalizi yamefikia wapi? Na nini kitajiri? Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa imewaalika wadau wa Kiswahili hapa kwenye makao makuu kufahamu maandalizi yanaendeleaje.

Wakimbizi wanendelea kuwasili Ethiopia baada ya kukimbia mapigano nchini Somalia.
© UNHCR/Muluken Tadesse

Ukata ni changamoto ya kuwasaidia wakimbizi wa Somalia walioko Ethiopia: UNHCR

Ethiopia inakabiliwa na dharura nyingi huku kukiwa na changamoto kubwa ya  ufadhili duni limeonya leo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na kuongeza kuwa huku kukiwa na watu wapya na wanaoendelea kutawanywa  na kuteseka kutokana na ukame, nchi hiyo ya Afrika Mashariki inahaha kukidhi mahitaji yanayoongezeka ya watu waliokimbia makazi yao nchini kote.