Dola mili 84 zaomba kushughulikia wahamiaji wanaotoka pembe ya Afrika Kwenda kusaka maisha ulaya
Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM, na washirika wengine 47 wanatoa ombi la dola milioni 84 ili waweze kutoa msaada wa kibinadamu na maendeleo kwa zaidi ya wahamiaji milioni 1 na jamii zinazowakaribisha, ambao wengi wao wako katika mazingira magumu, na wanahitaji msaada wa haraka na wa pamoja.