Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au coronavirus">COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Radio ya UN yawa kiungo cha wanafunzi na elimu wakati wa COVID-19 Sudan kusini
Radio Miraya inayoendeshwa na mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMIS imekuwa chombo muhimu cha kuhakikisha wanafunzi wanaendelea kupata elimu kupitia vipindi vya redio wakati huu shule zikiwa zimefungwa kutokana na janga la COVID-19 nchini .
Mshikamano na Afrika ni muhimu ili kusongesha maendeleo yaliyopatikana- Guterres
Ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 ukiendelea kusambaa barani Afrika, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amependekeza hatua za kisera za kusaidia bara hilo kukabiliana na changamoto zitokanazo na janga hilo ambalo hadi sasa limesababisha vifo vya watu 2500 barani humo.
Tathimini huru yahitajika dhidi ya hatua za WHO za kupambana na COVID-19: Azimio
Nchi wanachama 194 wa shirika la afya duniani WHO leo wamepitisha azimio la kutaka tathimini huru ya hatua za kimataifa za kupambana na janga la virusi vya corona au COVID-19 . Tathimini hiyo itamulika natua za shirika la Umoja wa Mataifa WHO lakini pia sio peke yake.
19 Mei 2020
Hii leo tunamulika COVID-19 na athari zake kwa watu wasio na chakula ambapo ripoti inasema umaskini utaua watu zaidi kuliko virusi vyenyewe. Kuelekea siku ya nyuki duniani kesho, tumezungumza na wanahabari wanaofuga nyuki Tanzania. Nchini Kenya madhehebu ya kikatoliki yaunga mkono upanzi wa miti, makala tunatamatishia huko Kakonko mkoani Kigoma na mashinani tunabisha hodi Kenya. Mwenyeji wako ni Flora Nducha.
Njaa kuongezeka mara mbili Afrika Mashariki na Pembe ya Afrika sababu ya COVID-19:WFP
Ripoti mpya iliyotolewa na shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP, kuhusu athari za kijamii na kiuchumi za janga la corona au COVID-19, imeonyesha kuwa tatizo la njaa linaweza kuongezeka zaidi ya mara mbili katika enchi za Afrika Mashariki na Pembe ya Afrika katika miezi mitatu ijayo.
Janga la COVID-19 ni kengele ya kutuamsha sote:Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema janga la virusi vya corona ni kengele ya kutuamsha sote hivyo ni wakati wa kushikamana na kusaka kinga na tiba ya kuutokomeza ugonjwa huu unaoiyumbisha dunia.
IAEA yapokea zaidi ya dola milioni 4 kusaidia nchi kupambana na COVID-19
Mpango wa shirika la kimataifa la nishati ya atomiki, IAEA wa kusaidia kutokomeza ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19, umepata msukumo mpya baada ya kampuni ya kijapani ya kutengeneza dawa, TAKEDA kuchangia zaidi ya dola milioni 4.7.
COVID-19 yaongeza chumvi katika kidonda cha LGBTI
Hii leo dunia inaadhimisha siku ya kimataifa ya kupinga chuki dhidi ya wapenzi wa jinsia moja, waliobadili jinsia na wale wenye wapenzi wa jinsia zote, IDAHOT, katika changamoto kubwa, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake wa siku hii ya leo 17 Mei.
Tuhakikishe hakuna anayeachwa nyuma kwenye huduma za mtandao- Guterres
Kuelekea siku ya kimataifa ya mawasiliano na habari kesho Mei 17, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa ujumbe wake wa siku hii akisema kuwa teknolojia ya habari inaweza kuwa nguzo ya matumaini, kwa kuwezesha mabilioni ya watu duniani kote kuwasiliana.
MINUSCA yapata msaada wa mashine ya kupima COVID-19 kutoka Rwanda
Kikosi cha Rwanda kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kuweka utulivu nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, MINUSCA kimepatia maabara ya kitaifa ya kibayologia nchini humo mashine yenye thamani ya dola 200,000 kwa ajili ya kupima ugonjwa virusi vya Corona au COVID-19.