IAEA yapokea zaidi ya dola milioni 4 kusaidia nchi kupambana na COVID-19
IAEA yapokea zaidi ya dola milioni 4 kusaidia nchi kupambana na COVID-19
Fedha hizo kutoka kampuni hiyo ambayo ni moja ya kampuni kubwa za kutengeneza dawa duniani, utawezesha IAEA, kuongeza msaada wake wa dharura kwa nchi wanachama ambazo zinahitaji mbinu za haraka na za kisasa za kudhibiti virusi hivyo ambavyo hadi sasa vimesababisha vifo vya zaidi ya watu 3,000,000 duniani kote.
Mapema mwezi Machi mwaka huu, IAEA ilitangaza kupatia nchi zitakazoomba msaada, mashine salama za kuchunguza virusi vya Corona sambamba na ushauri wa kitaalamu na muongozo wa kiufundi.
Hadi sasa mataifa 119 yameshawasilisha maombi yao IAEA yakitaka kutumia teknolojia ya nyuklia ambayo ni ya uhakika zaidi katika kutoa majibu ndani ya saa chache.
Ukurasa kuhusu virusivyacorona & taarifa mpya
Wasomaji wanaweza kupata taarifa na muongozo kuhusu mlipuko wa virusi vya corona (2019-nCoV) kutoka Umoja wa Mataifa, Shirika la afya duniani na mashirika mengine ya UN hapa. Kwa habari mpya kila siku kutoka UN News, bofya hapa.Mataifa 16 kati ya hayo tayari yamepokea mashine, vifaa vya kujikinga, na vifaa vya maabara na mataifa mengine yatapokea misaada ya aina hiyo siku na wiki chache zijazo.
Nchi ambazo zimeshapokea msaada huo ni pamoja na Morocco,Bosnia na Herzegovina, Burkina Faso, Iran, Latvia, Lebanon, Malaysia, Nigeria, Peru, Senegal, Thailand na Togo.
Akizungumzia mchango wa TAKEDA, ambao ni mkubwa zaidi kuwahi kutolewa na kampuni hiyo kwa wakati mmoja, Mkurugenzi Mkuu wa IAEA, Rafael Mariano Grossi amesema, “mchango wa TAKEDA uwezesha IAEA kuongeza kasi ya kusaidia dunia kukabili janga la Corona na kupeleka vifaa vingi zaidi vya uchunguzi kwa nchi ambazo zinahitaji.”
Amesema mchango huo unaongezea kwenye bajeti ya ziada ya dola zaidi ya milioni 23 ambazo tayari nchi 23 wanachama wa shirika hilo wameshaahidi kwa ajili ya kusaidia IAEA kukabili COVID-19.
Mradi huu wa sasa, ni mradi mkubwa zaidi wa ushirikiano wa IAEA kwa kiwango cha fedha na idadi ya wanufaika tangu shirika hilo lianzishwe mwaka 1956.
Bwana Grossi amesisitiza kuwa ana imani kuwa wataweza kukabili janga la Corona kwa pamoja.