Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au coronavirus">COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
WHO na Wizara ya afya Sudan Kusini washughulikia unyanyapaa unaowakumba hadi wanaompana na COVID-19
Unyanyapaa unaotokana na uoga ni moja ya vikwazo katika kudhibiti janga la COVID-19 na vimeshuhudiwa na wanajamii na pia wafanyakazi na mamlaka wanaopambana na COVID-19 nchini Sudan Kusini, inaeleza taarifa iliyotolewa hii leo mjini Juba na shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO.
Mwelekeo wa COVID-19 kwa nchi nyingi uko kisegemnege – Dkt. Tedros
Shirika la afya la Umoja wa Mataifa , WHO limesema kuwa mataifa mengi zaidi yana mwelekeo usio sahihi katika kupambana na ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19.
Wimbo maarufu One Love wa Bob Marley kutengenezwa upya ili kuiunga mkono 'Reimagine' ya UNICEF
Wanafamilia wa mwanamuziki nguli na wa kukumbukwa sana duniani, Bob Marley, wametangaza kuutengeneza upya wimbo maarufu wa Bob Marley unaofahamika kwa jina One Love ili waunge mkono kazi za shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, kurejesha tena ulimwengu wa haki zaidi kwa watoto ambao maisha yao yamevurugwa na janga la COVID-19, imeeleza taarifa ya UNICEF iliyotolewa hii leo mjini New York Marekani.
Nchi za Amerika Kusini na Karibea sasa ni kitovu cha janga la COVID-19, zisaidiwe-Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe wake wa kuzindua tamko la kisera kuhusu madhara ya corona au COVID-19 kwa eneo la Amerika Kusini na Karibea ameisihi jumuiya ya kimataifa kuzisaidia nchi za ukanda huo ili zisitetereke zaidi.
08 JULAI 2020
Katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea
-Janga la COVID-19 laongeza usafirishaji haramu wa vifaa tiva visivyokidhi viwango au bandia duniani imesema ripoti iliyotolewa leo na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya madawa na uhalifu UNODC
-Nchini Sudan Kusini wapiganaji wa makundi mbalimbali walioletwa pamoja ili kujiunga na mafunzo ya kuingia katika jeshi la kitaifa karibu wanahitimu
Tumepokea notisi ya Marekani kujitoa WHO ifikapo 2021- UN
Umoja wa Mataifa umesema umepokea taarifa ya serikali ya Marekani ya kujitoa rasmi kwenye shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO.
Wakimbizi raia wa DRC zaidi ya 3,000 wamewasili Uganda ndani ya siku tatu
Zaidi ya wakimbizi 3,000 raia wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC wamewasili Uganda kati ya Alhamis na Ijumaa ya wiki iliyopita yaani Julai 1-3 wakati wa kufunguliwa kwa muda kwa vituo viwili vya mipakani, Galajo na Mlima Zeu, kaskazini magharibi mwa Uganda, limeeleza hii leo mjini Geneva Uswisi, shirika la Umoja wa Mataifa la kushughulikia wakimbizi, UNHCR.
Afrika magharibi na kati, wasio na uhakika wa chakula wanaweza kuongezeka zaidi ya maradufu kutokana na COVID-19
WFP kupitia msemaji wake hii leo mjini Geneva Uswisi limesema changamoto za kijamii na kiuchumi zilizoletwa na njia zilizolenga kudhibiti kusambaa kwa COVID-19, zimeathiri kwa kiasi kikubwa uhakika wa chakula Afrika ya kati na magharibi.
Kundi la kwanza la raia 15,000 wakirejea, Sudan yaongeza huduma za kiafya katika vituo vya kuingilia
Taarifa iliyotolewa hii leo mjini Khartoum, Sudan na shirika la uhamiaji la Umoja wa Mataifa, IOM inaeleza kuwa serikali ya Sudan kuanzia mwezi uliopita,ikishirikiana na IOM imeanza kuratibu kurejea nyumbani kwa kundi la kwanza la raia wanaokadiriwa kufikia 15,000 ambao walikuwa wamekwama katika mataifa mengine.
Mwalimu aeleza changamoto za kiuchumi na kijamii kutokana na COVID-19, Uganda
Elimu bora kwa wote ni miongoni mwa malengo ya maendeleo endelevu au SDGs, lengo ambalo limeingia mashakani kutokana na mlipuko wa COVID-19 kwani serikali nyingi zimelazimika kufunga taasisi za elimu zote kama njia za kuudhibiti. Tuelekee nchini Uganda ambako John Kibego amezungumza na Mwalimu Charles Okuta, mmoja wa walimu waliochaguliwa kutoa mafunzo kwa njia ya redio katika wilaya ya Bwikwe kwa msaada kutoka shirika la World Vision tawi la Bwikwe.