Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au coronavirus">COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Familia za raia wa Nigeria ambao tayari wameathiriwa na migogoro, na sasa COVID-19, ‘wako mahututi’
Msaada na ufadhili vinahitajika haraka kwa mamilioni ya watu nchini Nigeria kwa watu ambao wamepigwa vikali na madhara ya mlipuko wa virusi vya corona au COVID-19 zikiwemo jamii zinazotegemea misaada kuishi kaskazini mashariki mwa nchi kutokana na migogoro, imesema hii leo ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia misaada ya dharura, OCHA.
Mabaharia zaidi ya 150,000 wakwama melini sababu ya COVID-19:ILO
Mabaharia wanapaswa kuchukuliwa kama wafanyakazi muhimu hivyo wanastahili kuruhusiwa kurejea nyumbani -limesema leo shirika la kazi duniani ILO, wakati likitoa wito wa hatua za haraka za kuwaachilia mabaharia kati ya 150,000 hadi 200,000 waliokwama kwenye meli kote duniani kwa sababu ya hatua za kukabiliana na janga la virusi vya corona au COVID-19.
Nyongeza ya dola milioni 40 kusaidia DRC kukabili dharura za kiafya ikiwemo Ebola
Umoja wa Mataifa umetoa dola milioni 40 kwa ajili ya kusaidia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ikabiliane na dharura za kiafya zinazokabili taifa hilo, ikiwemo ugonjwa wa Ebola na Surua.
Waandamanaji wanapaswa kujilinda, na kuwalinda wengine dhidi ya COVID-19-WHO
Waandamanaji ambao wanataka kwenda mitaani ili kupaza sauti zao ambazo wanataka zisikike, wanatakiwa kuchukua kila tahadhari ya kutokuambukizwa virusi vya corona au kuwaambukiza wengine, katika kipindi hiki ambacho bado mlipuko huu haujakaribia mwisho wake, limesema shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO.
05 JUNE 2020
COVID-19 yakwamisha harakati za kulinda wanyamapori- WWF
Wakati dunia hii leo ikipaza sauti kuhusu utunzaji wa bayonuai ikiwemo viumbe vilivyomo duniani, nchini Tanzania harakati za kulinda wanyama walio hatarini kutoweka wakiwemo tembo na faru weusi ziko hatarini kutokana na ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19 uliokumba dunia tangu mwezi Machi mwaka huu.
Vitendo vya uharibifu wa mazingira vyasababisha mazingira kutuma ujumbe - Guterres
Mazingira yanatutumia ujumbe dhahiri ya kwamba tunaharibu mazingira yetu ya asili kwa hasa yetu wenyewe, hivyo ndiyo alivyoanza Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake wa siku ya mazingira duniani hii leo Juni 5, maudhui yakiwa bayonuai.
Tanzania na Kenya miongoni mwa wanufaika wa fuko la mazingira duniani, GEF
Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo, FAO, hii leo limekaribisha hatua ya fuko la mazingira duniani, GEF, ya kutenga dola milioni 174 kwa ajili ya miradi 24 inayoshughulikia shaka na shuku za kilimo na mazingira katika mataifa 30 duniani.
Chanjo ni muhimu lakini pekee haitoshi:Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameuambia mkutano wa kimataifa kuhusu chanjo unaofanyika leo kupitia njia ya mtandao kwamba chanjo ni muhimu sana na imeokoa maisha ya mamilioni ya watu duniani lakini peke yake haitoshi kukabiliana na majanga makubwa ya kiafya kama linaloisumbua dunia hivi sasa la COVID-19.
Mradi wa sabuni wa wakimbizi wa Mali wawa mkombozi wa COVID-19 Niger:UNHCR
Wakimbizi wa Mali nchini Niger wanapambana na janga la virusi vya corona au COVID-19 kwa kutengeneza na kugawa sabuni na dawa ya kutakasa madoa baada ya kupatiwa mafunzo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR.