Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mwalimu aeleza changamoto za kiuchumi na kijamii kutokana na COVID-19, Uganda

Mwalimu aeleza changamoto za kiuchumi na kijamii kutokana na COVID-19, Uganda

Pakua

Elimu bora kwa wote ni miongoni mwa malengo ya maendeleo endelevu au SDGs, lengo ambalo limeingia mashakani kutokana na mlipuko wa COVID-19 kwani serikali nyingi zimelazimika kufunga taasisi za elimu zote kama njia za kuudhibiti. Tuelekee nchini Uganda ambako John Kibego amezungumza na Mwalimu Charles Okuta, mmoja wa walimu waliochaguliwa kutoa mafunzo kwa njia ya redio katika wilaya ya Bwikwe kwa msaada kutoka shirika la World Vision tawi la Bwikwe.

Audio Credit
Loise Wairimu/John Kibego
Audio Duration
3'14"
Photo Credit
UNICEF/Habib Kanobana