Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
COVID-19 ni jaribio kubwa la uongozi duniani- Bachelet
Kamishna Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Michelle Bachelet amesema janga la ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19 ni jaribio kubwa sana la uongozi hivi sasa.
Wawekeni wanawake na wasichana katika kitovu cha mapambano dhidi ya COVID-19: Katibu Mkuu wa UN
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo Alhamis ameonya kuwa hatua zilizopigwa katika usawa wa kijinsia na haki za wanawake vilivyofikiwa kwa miongo kadhaa, viko hatarini kurejea nyuma kutokana na mlipuko wa virusi vya corona, COVID-19.
Sehemu ya kunawa mikono hosptiali ya taifa Muhimbili, Tanzania yasaidia vita dhidi ya COVID-19
Wakati visa vya virusi vya corona vikiendelea kupanda kila uchao, mataifa yanahaha kuweka mikakati kuhakikisha kwamba yanalinda wananchi wake dhidi ya ugonjwa huo ambao umesambaa kote ulimwenguni huku ukisababisha vifo vya maelfu ya watu duniani kote.
Tuna wajibu wa kulinda wakimbizi dhidi ya COVID-19-UNHCR
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limesema linachukua tahadhari zote na kufanya kila liwezalo ili kuwalinda dhidi ya janga la virusi vya Corona, COVID-19 wakimbizi walio katika kambi mbalimbali za wakimbizi barani Afrika . Jason Nyakundi na taarifa zaidi
(TAARIFA YA JASON NYAKUNDI)
Nats…….
UNHCR yachukua tahadhari kabla ya hatari ya COVID-19 kulinda wakimbizi warohingya
Pamoja na kuwa hakuna mgonjwa yeyote wa virusi vya corona, COVID-19 ambaye ameripotiwa miongoni mwa wakimbizi nchini Bangladesh, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR linachukua hatua za kujiandaa kukabiliana na mlipuko ikiwemo kujenga wodi za kuwatibu wagonjwa katika maeneo hayo. Taarifa zaidi na John Kibego.
(Taarifa ya John Kibego)
Ni katika kambi ya wakimbizi ya Kutupalong nchini Bangladesh, wafanyazi wajenzi wako katika harakati za kukimbizana na muda, wengine wanafunga mianzi na wengine wanachanganya mchanga.
9 Aprili 2020
Assumpta Massoi : Hujambo na Karibu kusikiliza Jarida kutoka Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa, kutoka hapa New York Marekani.
JINGLE (04”)
ASSUMPTA:Ni Alhamisi 09 Aprili mwaka 2020, mwenyeji wako studioni hii leo ni mimi ASSUMPTA MASSOI
Kitabu cha watoto chazinduliwa kuwaelimisha kuhusu COVID-19
Zaidi ya mashirika 50 ya kibinadamu yakiwemo yale ya Umoja wa Mataifa yameandaa kitabu kipya cha kusaidia watoto kuelewa na kufahamu kwa kina ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19.
UNHCR yajipanga mapema kudhibiti COVID-19 katika kambi za wakimbizi wa Rohingya
Pamoja na kuwa hakuna mgonjwa yeyote wa virusi vya corona, COVID-19 ambaye ameripotiwa miongoni mwa wakimbizi nchini Bangladesh, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR linachukua hatua za kujiandaa kukabiliana na mlipuko ikiwemo kujenga wodi za kuwatibu wagonjwa katika maeneo hayo.