Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

23 Februari 2022

Karibu kusikiliza jarida ambapo leo tutakuletea mada kwa kina kutoka viziwani Zanzibar nchini Tanzania , ambapo ikiwa imesalia chini ya miaka 8 kufikia ukomo wa malengo ya amendeleo endelevu SDG’s juhudi zinafanyika kwa hali na mali kuhakikisha jamii zinafikia malengo hayo. Miongoni mwa wanaharakati wa kupigia upatu malengo hayo ni mke wa Rais wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar Bi. Mariam Mwinyi ambaye mwishoni mwa wiki amezindua wakfu au taasisi maalum ijulikanayo kama “Zanzibar Maisha Bora Foundation”.

Sauti
15'32"