Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

12 Novemba 2021

Karibu kusikiliza jarida ambapo leo Mada yetu kwakina inatokea huko Glasgow Scotland ambapo mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mkataba wa  mabadiliko ya tabianchi COP26 ukiwa unafunga pazia mwanaharakati wa Mazingira Dkt. Sixbert Mwanga kutoka nchini Tanzania anasema Afrika pamoja na kuwa na kauli moja lakini haijafanikiwa kwenye mkutano huo.

Pia utasikia habari kwa ufupi na kupata fursa ya kujifunza kiswahili .

Sauti
9'56"