Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Watoto wakimbizi wa ndani katika kambi ya Aden wakiwa wameshika vidumu vya maji. Kambi hiyo hutoa maji mara mbili kwa siku
UN OCHA/GILES CLARKE

Watoto bilioni 1 wako hatarini kwa athari za mabadiliko ya tabianchi:UNICEF Ripoti

  • Walio katika hatari zaidi ni kutoka Jamuhuri ya Afrika ya Kati, Chad, Nigeria, Guinea, na Guinea-Bissau
  • Mtoto 1 kati ya 3 ulimwenguni wanaishi katika maeneo ambayo angalau majanga manne ya mabadiliko ya tabianchi na mazingira yapo au yanaingiliana.
  • Mtoto 1 kati ya 7 duniani kote wanaishi katika maeneo yaliyoathiriwa na majanga makubwa matano. 

Jarida 20 Agosti 2021

Hii leo katika jarida utasikia mahojiano na manusura wa Covid-19, Bwana Ole Pertet, mmoja wa wakazi wa Marekani waliougua mwanzoni kabisa ugonjwa huo ulipoingia Marekani. 

Lakini kabla ya mada hiyo utasikia habari kwa ufupi ambapo kuelekea siku ya kimataifa ya kumbukumbu na kuwaenzi waathirika wa ugaidi, itakayoadhimishwa hapo kesho Agost 21, leo kwenye makao Makuu ya Umoja wa Mataifa kumefanyika mkutano wa ngazi ya juu kuwaenzi waathirika hao ukijikita  zaidi katika msaada wa kisaikolojia na ulinzi kwa waathirika.  

Sauti
11'16"