Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Baadhi ya maeneo ya Niger yameharibiwa kutokana na matumizi mabaya ya ardhi yasiyo endelevu.
©FAO/Giulio Napolitano

IFAD yasaidia wanawake wa Mouradi, Niger kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi

Nchini Niger, mfuko wa maendeleo ya kilimo wa Umoja wa Mataifa, IFAD kwa kushirikiana na serikali unasaidia wazalishaji wadogo wa nafaka hususani vikundi vya wanawake katika eneo la Mouradi ambao mabadiliko ya hali ya hewa yameathiri sana maisha yao ili waweze kukabiliana na hali inayobadilika na pia majanga ya baadaye.

Sauti
2'40"