Neno la Wiki - Si ndiyo
Katika neno la wiki Februari 3 tunachambua neno si ndiyo, mchambuzi wetu leo ni, Nuhu Zuberi Bakari ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA.
Katika neno la wiki Februari 3 tunachambua neno si ndiyo, mchambuzi wetu leo ni, Nuhu Zuberi Bakari ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA.
Wiki hii tunaangazia neno "Madhabahu" na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.
Bwana Sigalla anasema neno hilo lina maana tatu. Maana ya kwanza ikiangazia pahala takatifu, maana ya pili ni pahala pa kufanyia tambiko na maana ya tatu ni pahala pa kuchinjia wanyama.
Katika neno la wiki Februari 17 tunachambua maneno yanayotumika kama kitenzi, mchambuzi wetu leo ni, Nuhu Zuberi Bakari ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA.
Bwana Nuhu anasema kwamba kuna maneno yanyotumika kwenye lugha ya Kiswahili lakini hayapo ila tu yanatumika kihisi kama njia ya kusisitiza, anatolea matamshi ya baadhi ya maneno na jinsi matamshi yanaonyesha msisitizo
Wiki hii tunaangazia neno Keneka na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.
Kulingana na Bwana Sigalla neno hili lina maana zaidi ya moja, kwanza kama nomino, ala ya mziki ya kienyeji yenye vijiwa vinavotiwa katika mkebe, nyingine ni kuwa nyuma na wakati na chelewa nyingine kama nomino ni hali anayoiona mlevi baada ya kulewa jana, jina jingine ni maluweluwe.
Katika neno la wiki Februari 3 tunachambua maneno yamkini na yakini, mchambuzi wetu leo ni, Nuhu Zuberi Bakari ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA.
Bwana Bakari anasema kwamba neno yamkini maana yake kutokuwa na uhakika na jambo au kitu kufanyika, pengine, labda. Anaongeza kwamba asili ya neno hili ni kiarabu na kwa hiyo watu wa Pwani iwe Kenya au Tanzania wanatumia neno yumkini. Kinyume cha yamkini ni yakini, yakini ina maana ya uhakika.
Wiki hii tunaangazia neno “Aghalabu” na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.
Aghalab ni kama kielezi na inatumika kumaanisha "mara nyingi, au kwa kawaida au mara kwa mara". Mfano ya matumizi ya neno Aghalab kwa sentensi ni "Nyota nyingi aghalab huonekana usiku" Neno hili lina vinyume vyake kwa mfano nadra, adhimu au mara chache.
Watu wengine hutumia neno hili kimakosa, mara nyingi kumaanisha mara chahe au nadra
Wiki hii tunaangazia neno Keneka na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.
Kulingana na Bwana Sigalla, keneka ina maana ya kugeuza maji kuwa mvuke kwa kuchemsha na kisha kukusanya matone ya mvuke uliopita na kuwa maji maji.
Huu ni mchakato wa kisayansi ambao unafanyika ili watu waweza kupata maji yaliyoondolewa ikiwemo chumvi ili kupata maji safi ya kunywa.
Katika neno la wiki Januari 6 tunachambua maneno Tovuti na Wavuti, mchambuzi wetu leo ni, Nuhu Zuberi Bakari ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA.
Bwana Nuhu anasema kwamba maneno haya yanatumika vivyo sivyo kwani Tovuti ni intaneti na wavuti ni website.
Katika neno la wiki tunachambua neno "Mede", mchambuzi wetu leo ni Nuhu Zuberi Bakari ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa Maswala ya Mawasiliano kwenye Chama cha Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA.
Mede ina maana mbili, moja ni sehemu ya nyumba ambayo imetengwa kwa ajili ya kupumsikia, yaani kupiga gumzi au kupumsikia na wageni maalumu kando na chumba cha kupumsikia na familia ya kwako. Pili, Mede ni mchezo wa watoto wa kujificha ili wenzake wamtafute, yaani wanaweza kujificha chini ya kitanda au sehemu nyingine ya siri.
Wiki hii tunaangazia neno "Fila" na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.
Neno Fila ina maana mbili, ya kwanza neno hili hutumika katika msemo kwa maana ya "Ubaya" kwa mfano Lila na Fila haitangamani kumaanisha wema na ubaya havisikilizani, pili, Fila ni kifaa kinachotumiwa kujazia wino kwenye mashine ya chapa.