Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UNDP SGP Panama/Andrea Egan

Wanawake wa kijijini huko Karagwe mkoani Kagera nchini Tanzania wachukua hatua kulinda tabianchi

Oktoba 15 ni siku ya kuwaenzi wanawake wa vijijini kutokana na mchango wao katika sekta mbalimbali za jamii. Kaulimbiu ya mwaka huu wa 2019 imejikita katika kuangazia jukumu muhimu walilonalo wanawake wa vijijini na wasichana katika kujenga mnepo wa kukabiliana na hali ya hewa. Kulingazia hilo, Tumaini Anatory wa redio washirika Karagwe FM ya mkoani Kagera Tanzania ametembelea kijiji cha Bisheshe na kuzungumza na wanawake walioamua kuendesha kilimo kinachojali mazingira na hali ya hewa.

Sauti
3'33"
UN News/ John Kibego

Kenya yahaha kulinda mazingira dhidi ya taka ya mafuta

Rasilimali ya mafuta huleta matumaini ya ukuaji wa uchumi wa nchi husika kwani utafutaji, uchimbaji na usafishaji wake huleta fursa nyingi zikiwemo ajira kupitia ukuaji wa viwanda. Lakini kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa  sekta ya mafuta pia  huhatarisha mazingira na afya kutokana na hewa ukaa ya viwandani na taka za mafuta amabyo hujumuisha madini mazito kama zebaki endapo masuala ya mazingira hayashughulikiwi ipasavyo.

Sauti
4'3"
UNZimbabwe/2018

Kuelekea ICPD 25, Zimbabwe yachukua hatua madhubuti kunusuru vifo vya wanawake na watoto wa kike

Miaka 25 iliyopita huko Cairo Misri nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa waliazimia kupunguza na hatimaye kutokomeza vifo vya wanawake, wajawazito, watoto wachanga na watoto ili hatimaye dunia hii iwe na ustawi kwa wote bila kujali mtu anaishi eneo gani. Mataifa yalichukua hatua kwa kuzingatia kuwepo kwa mazingira hatarishi si tu kwa mama mjamzito na mtoto anayejifungua bali pia mila potofu na mazingira yanayomuozesha mapema mtoto wa kike na kumnyima haki ya kupata huduma za uzazi wa mpango. Sasa mataifa ikiwemo Zimbabwe yamechukua hatua, je yamefanya nini?

Sauti
3'30"
UNICEF/Rebecca Vassie

Kenya tunajitahidi kuwajumuisha wenye ulemavu katika maendeleo-Seneta Mwaura

Ujumuishwaji wa kila mtu katika jamii ndio nguzo ya kuhakikisha hakuna ayakayeachwa nyuma katika mchakato wa utimizaji wa ajenda ya mwaka 2030 ya maendeleo endelevu. Umoja wa Mataifa unasema mara nyingi makundi ya walio wachache katika jamii wakiwemo watu wenye ulemavu husahaulika na hivyo imezihimiza nchi kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha kundi hilo linajumuishwa na kupewa fursa. Miongoni mwa nchi zilizochukua hatua kuhakikisha hilo ni Kenya Ili kufahau kwa undani na ni hatua gani hizo?

Sauti
4'14"
UN/Assumpta Massoi

Napenda kufanya kazi na jamii ndio sababu najihusisha na kupigania usawa wa kijinsia- Thobias Komba

Msukumo wa kufanya kazi na jamii moja kwa moja umepelekea kijana Thobias Komba kutoka Tanzania kujihusisha na harakati za kuhakikisha usawa wa kijinsia kupitia shirikia lisilo la kiserikali la Restless Development nchini humo. Licha ya kwamba suala hilo linaolekana kama kujikita zaidi na wanawake au watu wa umri wa juu zaidi lakini kijana Komba anasema kufanya kazi katika jamii kunampa fursa ya kuielewa jamii zaidi na kuishi na jamii vizuri zaidi.

Sauti
3'49"
UN News/ Jason Nyakundi

Wanawake Nairobi wajitosa kutengeneza majeneza ili  kuinua kipato

Katika hatua za kuhakikisha usawa wa kijinsia jamii na wanawake wenyewe wanachukua hatamu kujitosa katika sehemu ambazo kawaida zilizoeleka kuendeshwa na wanaume . Mfano mmoja ni kazi ya useremala hasa ile ya kutengeneza majeneza ambayo kwa kawaida inajulikana kuwa ni kazi wanaume tu. Lakini Joyce Atieno na Eunice Atieno wote wanaoishi mjini Nairobi nchini Kenya, ni kati ya wanawake wachache ambao wamejiunga katika kazi hii na kuifanya kwa moyo wa kujitolea angalau wapate kukidhi mahitaji ya familia zao.

Sauti
5'6"