Nyanduga afarijika na jitihada za Somalia katika haki za binadamu
Awali wiki hii, waziri mkuu wa Somalia Omar Abdirashid Ali Sharmarke aliliteua Baraza jipya la mawaziri, wakati ambapo Somalia ilikuwa haina serikali tangu Desemba tarehe 6, mwaka 2014.
Hata hivyo, tarehe 20 mwezi Januari, bunge la Somalia limefanikiwa kuridhia mkataba wa haki za watoto, hatua hiyo ikibainiwa na watalaam kama dalili kubwa ya kuonyesha utashi wa serikali katika kuboresha hali ya watoto nchini.