Raia wa Guatemala anayejitolea Tanzania aeleza jinsi anavyoithamini kazi hiyo
Pakua
Leo ikiwa ni siku ya kimataifa ya kujitolea inaelezwa kuwa umuhimu wa siku hii ni katika kukuza amani na maendeleo duniani ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amesema mchango wa wanaojitolea unatambulika.
Miongoni mwa wanaojitolea ni Nataly Monila raia wa Guatemala anayefanya kazi za kufundisha mkoani Tanga nchini Tanzania na katika mahojiano na Muhamed Hamie wa radio washirika Pangani Fm, Bi Monila anasema licha ya kwamba hapati ujira kwa kazi anayofanya lakini anaifurahia kwani inatimiza ndoto zake.
(Sauti Mahojiano-Monila)