Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahojiano

Wahamiaji wa Kiethiopia na Kisomali wakwama Yemen IOM yaomba msaada

Shirika la kimataifa la uhamiaji, IOM nchini Djibouti  limetoa ombi la dharura la dola Milioni Tano kwa ajili ya kuokoa maisha ya wahamiaji wa Ethiopia na Somaliawalio kwenye mazingira magumu nchini humo baada ya kushindwa kuendelea na safari ya ughaibuni.

Msemaji wa IOM Jumbe Omari Jumbe amesema ombi la awali la dola Milioni 72 kwa Djibouti kupitia mchakato wa Umoja wa Mataifa bado halijatekelezwa na sasa wanahitaji haraka fedha hizo kukwamua wahamiaji hao walio kwenye ofisi ya IOM huko Obok nchini humo.

Boda boda zaendelea kukatiza uhai wa watu kwenye ajali barabarani

Ni hivi  karibuni tu shirika la afya duniani WHO lilitoa ripoti  inayoonesha kuwa ni mataifa 28 pekee yenye asilimia 7 ya watu wote duniani yana sheria madhubuti za usalama barabarani kwenye maeneo makuu matano ambayo ni kunywa pombe na kuendesha gari, mwendo kasi kupindukia, matumizi ya kofia kwa waendesha pikipiki, kufunga mikanda na matumizi ya viti maalum kwa watoto.

Unicef yapiga kambi Niger kukabiliana na utapiamlo

Mapigano yanayoendelea nchini Mali yamesababisha zaidi ya wakazi 270,000 wa nchi hiyo iliyoko Magharibi mwa Afrika kukimbilia nchi jirani kutafuta hifadhi. Hata hivyo wakiwa njiani wanakumbana na kadhia mbalimbali na watoto wa wanawake huathirika zaidi.  Nchini Niger, ambako yanapokelewa makundi ya wakimbizi kutoka Mali, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limelazimika kupiga kambi humo kusaidia kwa matibabu kutokana na magonjwa kadhaa, ukiwemo utapiamlo unaotokana na lishe duni. Basi kupata undani wa ripoti hiyo ungana na Joseph Msami.

Surua yatishia usalama wa watoto DRC Kongo,UNICEF yasaidia

Mapigano mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC pamoja na mambo mengine yametajwa kukwamisha jitihada za kukabiliana na hatimaye kudhibiti ugonjwa wa surua hususani mongoni mwa watoto.Hii inatokana na kwamba mapigano kati ya jeshi la serikali na waasi yamesababisha watu kukimbia makazi yao na kuishi katika makzi yenye msongamano .Jitihada za kutoa chanjo zinakwama!

Ajali za barabarani zamulikwa katika ripoti ya WHO

Shirika la afya duniani WHO limetoa ripoti mpya inayoonyesha kuwa ni mataifa 28 tu yenye asilimia saba ya watu wote duniani ambayo yana sheria madhubuti za usalama barabarani kwenye maeneo makuu matano ambayo ni muhimu  katika kupunguza ajali za barabarani. Je, ni nini sura ya bara la Afrika katika viwango vya ajali na usalama barabarani?

Ungana na Joseph Msami katika tarifa hii inayoangazia ripoti hiyo na mikakati ya kujikinga na ajali hizo zinazotajwa kupoteza maisha ya mamilioni ya watu duniani, wengi wao wakiwa kutoka Afrika

Sehemu za ibada zatumika kutoa tiba Uganda: UNICEF

Huduma ya afya ya msingi ni jambo muhimu kwa jamii ili waweze kushiriki shughuli za maendeleo. Hata hivyo katika maeneo mengi ya nchi zinazoendelea Uganda ikiwa ni mojawapo, watu hulazimika kwenda mwendo mrefu kupata huduma hizo na hivyo kusababisha kukosa huduma au kuipata wakati wameshachelewa. Kwa mantiki hiyo Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, limebuka na mpango mpya nchini Uganda. Je ni upi huo? Ungana na Joseph Msami katika ripoti hii.

MONUSCO yapambana na waasi DRC Kongo,juhudi zaidi zahitajika

Kongo DRC ni nchi ya pili kwa ukubwa barani Afrika yenye rasilimali nyingi, ikiwemo madini na uoto wa asili. Nchi hii yenye idadi ya zaidi ya watu milioni sabini ina historia ndefu ya mapigano yaliyosababisha maafa kadhaa ikiwamo vifo, ulemavu na hata wakimbizi wa ndani ya nchi na wale waliokimbilia nchi jirani kutafuta hifadhi.

Mwishoni mwa mwezi February umeripotiwa mapigano katika kijiji cha Kitchanga kati ya kundi la Wanamgambo linalofahamika kama Muungano wa Wazalendo kwa ajili ya Kongo iliyo huru na inayojitegemea (APCL) na jeshi la serikali ya Kongo DRC (FARDC).

Ushirikiano wahitajika kudhibiti wizi wa haki miliki: WIPO

Suala la haki miliki linaelezwa kuwa bado linaendelea kuzua utata na kukwamisha matumizi stahili ambayo yanaweza kusaidia nchi kujikwamua kiuchumi.

Barani Afrika ripoti zinaonyesha kuwa mapato mengi hupotea kutokana na kukithiri kwa vitendo vya wizi wa haki miliki, kunafanyika kwenye maeneo mbalimbali.

Ni kwa mantiki hiyo wataalamu wanakutana jijini Dar es Salaam katika mkutano ulioandaliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la hakimiliki, WIPO na serikali ya Tanzania. George Njogopa ametuma taarifa hii.

UNMISS yatoa mafunzo ya lugha ya kiingereza kwa polisi wa kike

Dunia ikiwa imeadhimisha siku ya wanawake Machi Nane ambapo tumeshuhudia maadhimisho hayo yakifanyika kwa matukio mbalimbali ikiwemo matembezi na kadhalika, nchini Sudan Kusini,Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo UNMISS, umetumia maadhimisho ya siku ya wanawake kwa kufundisha  Kiingereza  wanawake zaidi ya 50.  Mafunzo hayo yanafanyika katika hema lililoko katika karakana iliyoko katika kituo cha polisi Sudan Kusini ambapo askari wanawake wanaofundishwa lugha ya Kiingereza iliyo miongoni mwa lugha rasmi ya nchi  ni kutoka Jeshi la Polisi la nchi hiyo.Ungana na Joseph