19 JANUARI 2024
Hii leo jaridani tunaangazia vita katika ukanda wa Gaza, na tukielekea siku ya elimu duniani tunabisha hodi nchini Burundi ambako UNICEF inahakikisha watoto wakimbizi wanaorejea nchini humo wanaweza kuendelea na elimu. Makala na mashinani tunasalia na mada ya elimu bora na tunakupeleka nchini Uganda, kulikoni?.
17 JANUARI 2024
Jaridani leo tunamulika jukwaa la uchumi duniani mjini Davos Uswis, na suala la kilimo endelevu. Makala tnakuletea mbinu tatu zinazotumika kuhakikisha watoto na familia zao wanapata chanjo na mashinani tutabisha hodi mkoani Mbeya nchini Tanzania kusikia ujumbe kuhusu ujuzi unaohitajika ili kufundisha wanafunzi kwa ufanisi.
15 JANUARI 2024
Hii leo jaridani tunaangazia machafuko katika ukanda wa Gaza na Ufugaji nyukinchini Uganda. Makala tunarejea Gaza na mashinani tunakupeleka nchini Rwanda, kulikoni?
12 JANUARI 2024
Hii leo jaridani tunaangazia kesi mbele ya mahakama ya Umoja wa Mataifa ya kimataifa ya haki ICJ inayotaka Israeli kukomesha mauaji ya raia huko Gaza, na haki za wanawake za unyonyeshaji. Makala tunakupeleka nchini Ukraine na mashinani nchini Kenya, kulikoni?