Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

06 OKTOBA 2023

Hii leo jaridani mwenyeji wako ni Anold Kayanda akimulika pamoja na mambo mengine mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, Mabadiliko ya Tabianchi, vijana na siasa pamoja na majiko sanifu.

1.Kamati ya tuzo ya amani ya Nobel mwaka huu imemtunuku mfungwa mwanaharakati wa masuala ya haki za binadamu wa Iran Narges Mohammadi na Umoja wa Mataifa umepongeza uamuzi huo

Sauti
13'13"

05 OKTOBA 2023

Mwandishi wetu wa Kenya Thelma Mwadzaya ametembelea maktaba ya Little Voice Deep iliyoko jijini Nairobi kujionea jinsi gani kupitia waalimu walioko inavyochangia kuhakikisha watoto wanapata elimu wanayoitaka na kusongesha lengo namba 4 la malengo ya maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa linalohusu elimu bora.

Sauti
11'24"

04 OKTOBA 2023

Hii leo jaridani tunaangazia ripoti ya UNCTAD na elimu kwa watoto wote. Makala tunarejelea uchambuzi wa ibara ya 10 ya Tamko la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa. Mashinani tunakupeleka nchini DRC, kulikoni? 

Sauti
11'42"

03 OKTOBA 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina na inatupeleka Kibokoni, Kaunti ya Kilifi nchini Kenya ambako mabwawa ya samaki yamebadili kabisa maisha ya wavuvi wa eneo hilo walioathirika na mabadiliko ya tabianchi yaliyosabisha samaki kutoweka baharini na kuwakatisha tamaa ya Maisha. Lakini sasa kupitia mradi wa ufugaji samaki ulio chini ya mwamvuli wa Umoja Self-Help Group jamii hiyo ina mabwawa 17 ya samaki yanayozalisha samaki aina ya milkfish, kamba, kaa, sandfish, rabbitfish na perege au tilapia. Mshiani tanakuletea ujumbe kusu afya ya uzazi na uswa wa kijinsia. 

Sauti
11'35"

02 OKTOBA 2023

Hii leo jaridani tunaangazia siku ya kimataifa ya makazi, na simulizi ya wakimbizi wa Armania kutoka Karabakh. Makala tunakupeleka nchini Tanzania na mashinani nchini Kenya, kulikoni

Sauti
10'23"