Mtoto kuzaliwa njiti humtia hatarini kukumbwa na kifo, hatua zichukuliwe- WHO
Inakadiriwa watoto milioni 13.4 njiti (wanaozaliwa kabla ya wiki 37 za ujauzito) walizaliwa mwaka 2020 idadi hii ikiwa ni takriban mtoto 1 kati ya 10 na wengi wa watoto hao ni kutoka Ukanda wa jangwa la Sahara na Asia ya Kusini imesema ripoti iliyochapishwa leo kwenye jarida la masuala ya afya la Lancet. Leah Mushi na maelezo zaidi.