Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

17 AGOSTI 2022

Hii leo jaridani tunaanzia Yemen ambako shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO limepeleka misaada ya vifaa vya matibabu kwa ajili ya manusura wa mafuriko yaliyokumba taifa hilo. Kisha ni Pembe ya Afrika wanawake na watoto wakiwa katikati ya kukumbwa na janga la njaa wanakumbuka hali ilivyokuwa bora kabla ukame haujatumbukiza maisha yao kwenye hali tete. Makala tunabisha hodi mkoani Morogoro nchini Tanzania ambako huko wataalamu wanafafanua maana ya sumu kuvu na athari zake kiafya na kwenye mazao.

Sauti
9'57"

16 AGOSTI 2022

Hii leo jaridani tuna Habari kwa Ufupi zikiletwa kwako na Leah Mushi akimulika meli ya kwanza yenye shehena ya ngano kutoka Ukraine ikielekea Ethiopia ambako  huko ngano hiyo itasambazwa kwa wahitaji wa kibinadamu. UNICEF imetoa kandarasi ya kwanza ya kutengeneza chanjo za Malaria kwa ajili ya watoto. Kisha wito wa UNFP wa kutaka huduma za afya ya uzazi kwa wanawake na wasichana huko Haiti licha ya ghasia zinazoendeshwa na magenge ya  kihalifu.

Sauti
11'29"

15 AGOSTI 2022

Hii leo jaridani tunamulika mwaka mmoja wa watalibani madarakani nchini Afghanistani na madhara yake kwa watoto wa kike. “Watoto wa kike hawaruhusiwi kuendelea na masoko ya elimu ya sekondari.”
Kisha Sudan Kusini ambako walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanahaha kuondoa maji ya mafuriko yaliyotwama kwenye mji wa Bentiu, jimboni Unity.
Makala tunaye kijana Gloria Anderson Mkurugenzi wa shirika la TEDI Tanzania ambalo linahamasisha elimu inayoendana na hali ya sasa ya sayansi na teknolojia ili kuwaandaa wanafunzi kuanzia ngazi za chini kuweza baadaye kujiajiri na kuajiriwa.

Sauti
12'34"

12 AGOSTI 2022

Hii leo jaridani tunamulika siku ya vijana tukianza na ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akitaka vijana wajumuishwe na kubwa zaidi mfumo wa elimu urekebishwe. Kisha tunamulika furaha waliyoipata watu wa jamii ya kabila la washona nchini Kenya ambao baada ya kuhamia nchini humo miaka ya 1960 hatimaye wamepata uraia na kuweza kupiga kura. Makala tunamulika Kiswahili na tunakwenda DRC na Ujerumani. Mashinani ni ujumbe kwa vijana. Karibu na mwenyeji wako ni Assumpta Massoi.
Sauti
11'7"

11 AGOSTI 2022

Hii leo katika jarida tunamulika siku ya vijana duniani ambayo itaadhimishwa kesho Agosti 12 na tunakwenda Tabora nchini TAnzania kusikia sauti za vijana wakijibu wito wa maudhui ya mwaka huu ya ushirikiano baina ya marika yote ili kuwezesha kufikia malengo ya vijana kwa mujibu wa ajenda 2030 ya malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Mwenyeji wetu Tabora ni Happiness Pallangyo wa Radio washirika RAdio Uhai FM. Kuna Habari kwa Ufupi ikimulika wito wa UN kwa wananchi wa Kenya wakati huu wakisubiri matokeo ya uchaguzi mkuu.

Sauti
12'11"

10 AGOSTI 2022

Hii leo jaridani tunaanza na sarafu za kidijitali au Cryptocurrency kwa kiingereza ambapo Umoja wa Mataifa unatoa kuwa inatishia utulivu wa kifedha kutokana na ukosefu wa será za udhibiti na usimamizi. Sasa kupitia UNCTAD, UN inatoa miongozo ya kisera.

Sauti
11'59"

09 AGOSTI 2022

Hii leo jaridani tunaanza na siku ya kimataifa ya watu wa jamii ya asili duniani ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anapigia chepuo teknolojia zinazohamishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine na wanawake wa jamii ya asili. Kisha tunamulika kifaa cha kupatia hewa ya oksijeni watoto wachanga kilichotengenezwa Kenya na sasa kimepelekwa Ukraine kusaidia hospitali ambako vifaa hivyo ni nadra au havipo. Mashine haitumii umeme!

Sauti
9'50"

08 AGOSTI 2022

Hii leo jaridani tunaanza na habari kuhusu unyonyeshaji wa maziwa ya mama kwa mtoto na tunakwenda Morogoro nchini Tanzania. Kisha tunamulika harakati za FAO kuhakikisha kuwa wakulima wanapata pembejeo ili waweze kupanda mazao msimu huu wa Meher na kisha wavune Oktoba mwaka huu. Makala tunamulika kijana Suzan Yumbe na taasisi yao ya Afya Plus Tanzania na changamoto alizokumbana nazo kuelekea kuanzisha shirika hilo. Mashinani tunasalia Tanzania na ujumbe wa kijana Hussein Meleke kwa  vijana wa Kenya wanapokwenda kupiga kwenye uchaguzi mkuu kesho Agosti 9.

Sauti
10'38"

05 AGOSTI 2022

Hii leo jaridani tunaanzia huko Somalia ambako Umoja wa Mataifa umesihi jamii ya kimataifa ianze kutoa misaada ya kimkakati Somalia ambako ukame umeathiri wakulima ambao ndio wazalishaji wa chakula, hivyo misaada ianze kutolewa sasa. Kisha tunafunga safari hadi Thailand ambako teknolojia mpya ya kusafisha maji kwenye mabwawa ya kufugia kamba wadogo imesaidia kumaliza changamoto ya magonjwa ya mlipuko kutokana na  ulaji wa kamba waliochafuliwa na maji.

Sauti
11'1"

04 AGOSTI 2022

Hii leo jaridani kubwa ni mada kwa kina ikitupeleka nchini Kenya ambako mwandishi wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa Thelmwa Mwadzaya ametembelea shule inayosomesha watoto wa kike bila malipo, watoto ambao wako hatarini kukumbwa na ndoa za utotoni na ukeketaji au FGM. Nini kinfanyika? Na wazazi wanasemaje? 

Sauti
12'24"