Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

12 AGOSTI 2022

12 AGOSTI 2022

Pakua
Hii leo jaridani tunamulika siku ya vijana tukianza na ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akitaka vijana wajumuishwe na kubwa zaidi mfumo wa elimu urekebishwe. Kisha tunamulika furaha waliyoipata watu wa jamii ya kabila la washona nchini Kenya ambao baada ya kuhamia nchini humo miaka ya 1960 hatimaye wamepata uraia na kuweza kupiga kura. Makala tunamulika Kiswahili na tunakwenda DRC na Ujerumani. Mashinani ni ujumbe kwa vijana. Karibu na mwenyeji wako ni Assumpta Massoi.
Audio Duration
11'7"