Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

15 Februari 2022

Miongoni mwa yaliyomo 

Ikiwa leo ni siku ya Kimataifa ya saratani ya utotoni, 15 Februari 2022, Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni WHO barani ulaya limetoa ripoti inayoonesha kukosekana kwa usawa baina ya nchi na nchi kwa suala la saratani ya watoto katika Kanda ya Ulaya ya WHO. 

Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO laonya kuhusu ukame unavyoongeza zahma ya kutokuwa na uhakika wa chakula Pembe ya Afrika. 

Sauti
12'10"

14 Februari 2022

Miongoni mwa yaliyomo 

Ulimwengu ukiwa umeadhimisha siku ya redio duniani hapo jana na maudhui makuu yakiwa ni Imani kwa Radio, leo tunaiangazia redio iliyoanzishwa mnamo mwaka 1995 nchini Tanzania na huduma ya majesuit wa kikatoliki kwa wakimbizi (JRS), ili kuwakutanisha wakimbizi waliokuwa wamepoteana na jamaa zao wakati wa vita ya kimbari nchini Rwanda. 

Sauti
19'46"

11 Februari 2022

Miongoni mwa yaliyomo 

Kujaa maji kwa ziwa Albert nchini Uganda kwaleta zahma kubwa kwa wakazi, wengine wapoteza makazi, Umoja wa Mataifa nao wanyoosha mkono kusaidia. 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres asema kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya viwango vya chini vya wanawake wanaofanya kazi katika masuala ya Akili Bandia (AI), na kanuni za hovyo za upendeleo wa kijinsia. 

Sauti
12'38"

10 Februari 2022

Miongoni mwa yaliyomo  

Niger yapongezwa kwakuonesha ukarimu kwa wasaka hifadhi na wakimbizi. Viongozi wa mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa likiwemo lile la Kuhudumia wakimbizi UNHCR Filippo Grandi na lile la Uhamiaji IOM Antonio Vittorino wamefanya ziara nchini humo. 

Timu ya wataalamu kutoka ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuondokana na mabomu ya kutegwa ardhini, UNMAS pamoja na Mamlaka za Kitaifa wanafanya kazi kila siku nchini Sudan Kusini ili kuyadhibiti mabomu ambayo yako katika mazingira na hayajalipuka. 

Sauti
14'1"

09 Februari 2022

Miongoni mwa yaliyomo


Kuelekea siku ya kimataifa ya mikunde, vijana huko Kigoma kupitia mafunzo yaliyowezeshwa na Umoja wa Mataifa, wadhihirisha mikunde ni tija kiuchumi, kijamii na kimazingira.

Sauti
13'36"

08 Februari 2022

Miongoni mwa yaliyomo 

UNHCR, IOM, UNICEF na Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, OHCHR, wasikitishwa sana na taarifa za kifo cha mtoto mchanga kilichotokea Jumapili wakati wa walinzi wa mpaka wa pwani wa Trinidad walipokuwa wanakizuia chombo kilichowabeba wavenezuela waliojaribu kuvuka mpaka. 

Sauti
14'26"

07 Februari 2022

Miongoni mwa yaliyomo 

ikiwa ni siku moja baada ya ulimwengu kuadhimisha siku ya kimataifa ya kutokomeza ukeketaji wa wanawake na wasichana, FGM, tunaangazia harakati za Umoja wa Mataifa, wadau na wanaharakati katika kufanikisha kuelimisha umma kuhusu ubaya wa matendo hayo. 

Sauti
9'57"

Jarida 07 Februari 2022

Miongoni mwa yaliyomo 

ikiwa ni siku moja baada ya ulimwengu kuadhimisha siku ya kimataifa ya kutokomeza ukeketaji wa wanawake na wasichana, FGM, tunaangazia harakati za Umoja wa Mataifa, wadau na wanaharakati katika kufanikisha kuelimisha umma kuhusu ubaya wa matendo hayo. 

Sauti
9'57"

Jarida 04 Februari 2022

Miongoni mwa yaliyomo 


Leah Mushi amefanya mazungumzo na Dokta. Paul Mutungi Afisa wa mashinani wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO akihusika na wafugaji katika Ukanda wa Afrika wakiangazia suala la ukame na njaa kali unavyoathiri wananchi walioko Afrika Mashariki na pembe ya Afrika.


Mashindano ya Olimpiki ya majira ya baridi kwa mwaka huu wa 2022 yameng’oa nanga hii leo huko Beijing China huku Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akitoa wito wa mshikamano wakati wa michezo na hata baada.

Sauti
11'52"

Jarida 03 Februari 2022

Miongoni mwa yaliyomo


UNICEF yasaidia familia zinazokabiliwa na ukame na utapiamlo katika maeneo ya nyanda za chini nchini Ethiopia uliosababishwa na mvua kutonyesha katika misimu mitatu.


Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR linaendelea kufanya kila jitihada kuwasaidia wakimbizi na raia wa Lebanon ambao wanakabiliana na moja ya misimu yenye baridi kali. 

Sauti
12'7"