Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

UNMISS/Denis Louro

Kufanya kazi ya kujitolea ni kukumbatia jamii

Kutana na mfanyakazi wa kujitolea wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini Jason William Gbambi ambaye ni afisa uhamasishaji wa timu ya maadili na nidhamu ya mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo UNMISS. Anasema kufanya kazi ya kujitolea ni kukumbatia jamii na kutambua mahitaji yao na hasa amani ambayo ni adumu nchini humo. 

Sauti
2'36"
© UNICEF/Catherine Ntabadde

Afrika kusaidiwa Fedha na Benki ya dunia ili kununua chanjo

Katika kufanikisha lengo la Muungano wa Afrika, AU kuhakikisha asilimia 60 ya wakazi wa bara lake wamepatiwa chanjo dhidi ya ugonjwa wa Corona au COVID-19 ifikapo mwaka 2022, Benki ya Dunia na AU wametangaza ubia wa kuunga mkono mpango wa kikosi kazi cha Afrika cha kupata chanjo hizo, AVATT utakaoruhusu nchi za Afrika kununua na kusambaza dozi za chanjo kwa ajli ya watu milioni 400 barani kote. 

Sauti
1'55"
WFP/Falume Bachir

Mkimbizi wa ndani aishukuru WFP kwa msaada wa chakula.

Mkimbizi wa ndani Abbas Adu na wengine laki 4 wamelishukuru Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa chakula WFP kuwapatia msaada wa chakula wakati huu ambapo WFP imepaza sauti kwa wahisani kusaidia wananchi Milioni 41 wanaokabiliwa na njaa kutokana na hali mbaya ya hewa ambayo imeathiri mavuno yao na hivyo kukosa chakula.

Sauti
2'2"
UN Photo/Isaac Billy

Miaka 10 ya Uhuru Bado Sudan Kusini inahitaji msaada : Nicholas Haysom

Taifa changa zaidi duniani Sudan Kusini linaenda kutimiza muongo mmoja tangu kupata uhuru wake lakini Umoja wa Mataifa unasema bado kuna kazi kubwa ya kufanya kwani baadhi ya makubaliano hayatekelezwa, watu wenye nia ovu wanaendelea kuwatesa raia na wafanyakazi wa mashirika ya misaada nao wanavamiwa na kuuawa. 
Julai 9, mwaka 2011 Sudan Kusini ilijipatia uhuru wake baada ya kujitenga kutoka Sudan, na hivyo kuwa taifa changa zaidi duniani.  
 

Sauti
2'34"
©UNHCR/Vincent Tremeau

Zaidi ya Wananchi wa Venezuela Milioni 5.6 waikimbia nchi yao

Venezuela, ni moja ya Mataifa ambayo wananchi wake wanakimbia kwa wingi na kwenda kuomba hifadhi mataifa mengine ambapo takwimu za hivi karibuni zinaonesha takribani robo ya wananchi wake wamekimbia hali ambayo imefanya Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR kuitisha mkutano hii leo huko Canada ili kusaka suluhu ya kudumu. Tuungane na Leah Mushi kwa undani wa taarifa hii.

Sauti
2'57"