Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

UNHCR/Stephen Ferry

Wahamiaji wana haki na wanasitahili usaidizi bila kujali wanakotoka-Nick Ogutu

Mkutano wa 16 wa kuhusu haki za binadamu, uhamiaji na vijana leo umeingia siku yake ya pili katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. Mkutano huo wa kimataifa unaofanyika kila mwaka unawakutanisha wadau wa haki za binadamu kutoka kote duniani na mmoja wa waliohudhuria ni rais wa taasisi inayoitwa ‘Safari yangu’, inayosimamiwa na Chuo Kikuu cha Columbia cha hapa Marekani, Bwana Nick Ogutu.

Sauti
1'39"
MINUSMA/Gema Cortes

Washambuliaji wa raia Mali sasa kutokwepa sheria:MINUSMA

Nchini Mali, kufuatia mfululizo wa mashambulizi ya vijiiji na mauaji ya raia katikati mwa nchi hiyo, kitengo cha polisi wanasayansi kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kuweka utulivu kwenye taifa hilo la Afrika Magharibi wanafanya uchunguzi wa kina ili kuhakikisha hakuna ukwepaji wa sheria kwa watekelezaji wa mashambulio hayo.

Sauti
1'49"

27 Juni 2019

Miongoni mwa habari anazokuletea hii leo arnold Kayanda katika Jarida laletu ni pamoja na 

-Halahala yatolewa na shirika la afya ulimwenguni watu kupata chanjo ya surua kabla ya kwenda nchi zenye mlipuko wa ugonjwa huo

-Nchini Mali tunamulika masuala ya ukwepaji sheria dhidi ya wanaoshambulia raia , uchunguzi ukifanyika chini ya mpango wa umoja wa Mataifa MINUSMA

-Madhila anayosimulia mkimbizi toka Yemeni kuwa kila anakokimbilia na wanawe, ni kaburi tu

Sauti
12'43"
UN News/Matt Wells

Mitaji mikubwa kwenye biashara ndogo na za kati kufanikisha SDGs- ITC

Kuelekea siku ya biashara ndogo na za kati, SMEs hapo kesho, Umoja wa Mataifa umetaka uwekezaji zaidi kwenye biashara hizo kwa kuwa ndio msingi wa kufanikisha maleng ya maendeleo endelevu, SDGs. Flora Nducha na maelezo zaidi.

Kituo cha biashara cha kimataifa, ITC ambayo ni ofisi tanzu ya kamati  ya biashara na maendeleo ya Umoja wa Mataifa, UNCTAD, imesema hayo kupitia ripoti yake mpya iliyotolewa wiki hii ikisema kuwa msisitizo ni biashara ndogo na za kati kwa kuzingatia mambo makuu manne.

Sauti
2'7"
UNIS

"Back To Life" imebadili maisha ya waathirika wa madawa ya kulevya na kuwarejesha katika jamii- Masha Born

Hii leo ikiwa ni siku ya kupiga vita matumizi ya madawa ya kulevya duniani, vituo vya kusaidia waathirika wa madawa hayo vimekuwa msaada mkubwa wakati huu ambapo Umoja wa Mataifa unasema ya kwamba watu milioni 35 ulimwenguni kote wana matatizo yatokanayo na matumizi ya madawa hayo ilhali ni mtu 1 tu kati ya 7 ndiye anayepata matibabu. Assumpta Massoi na ripoti kamili.

Sauti
2'7"duration