Ban alaani mauaji ya mlinda amani wa UM nchini DRC
Imebainika kuwa mlinda amani aliyeuawa Jumatatu asubuhi huko Butembo, jimbo la Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ni kutoka Afrika Kusini.
Kufuatia taarifa hizo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amelaani mauaji hayo yaliyofanyika wakati wa makabiliano kati ya askari wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa DRC, MONUSCO na wapiganaji wanaosadikiwa kuwa wa Mai-Mai.
Katika makabiliano hayo walinda amani wengine wawili wa Afrika Kusini walijeruhiwa.