Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wanahabari Zanzibar watakiwa kukuza demokrasia na amani

Wanahabari Zanzibar watakiwa kukuza demokrasia na amani

Umoja wa Mataifa nchini Tanzania umevitaka vyombo vya habari visiwani Zanzibar, kutumia nafasi yake kukuza  demokarsia na amani wakati wa uchaguzi mkuu mwezi Oktoba mwaka huu.

Mwakilishi mkazi wa UM nchini humo Alvaro Rodriguez amewaambia wanahabari katika mkutano na vyombo hivyo leo kuwa jukumu la kuhakikisha  uchaguzi huru na wa amani sio wa tume ya uchaguzi na vyama vya siasa pekee na kutaka tasinia hiyo kuwa wajumbe wa amani na majadiliano.

Akizungumzia mafanikio ya Umoja wa Mataifa visiwani Zanzibar Rodriguez amesema mojawapo ni uwezeshaji wa  wanawake kushika nyadhifa  za kisiasa na kuanzishwa kwa redio za kijamaii zilizotumika kutoa elimu ya uraia pamoja na kuwa jukwaa la haki za wanawake na watoto.

Kwa upande wao waandishi wa habari wanazungumzia wajibu wao katika amani na demokarsia kulekea uchuguzi mkuu

(SAUTI)